Mabingwa wa soka wa Tanzania Bara, Yanga wameanza vyema
mzunguko wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuifunga mabingwa wa
Rwanda, APR mabao 2-1.
Katika mchezo huo
uliofanyika kwenye uwanja wa Amahoro,
Rwanda, APR, Yanga ilitawala kipindi chote cha kwanza na kuwafanya mashabiki wa
APR ambao wengi wao walikuwa ni wanajeshi kukaa kimya.
Kocha wa Yanga, Hans Van Pluijm alimpa unahodha mchezaji wa zamani wa APR, Haruna
Niyonzima, kitendo ambacho kiliwafanya mashabiki wa soka wa Rayon na klabu
nyingine kuishangalia Yanga na kuonekana kama ipo uwanja wa nyumbani.
Yanga ilianza kwa kasi katika mchezo huo na kupata bao
kwanza katika dakika ya 20 kupitia Juma
Abdul kwa mkwaju wa mita 25 baada ya mabeki wa APR kumfanyia faulo
Amissi Tambwe. Mpira huo wa faulo uliachwa na Niyonzima na
Thaban Kamusoko kabla ya Juma Abdul kufumua shuti kali na kumpita kipa maarufu
wa APR, Oliver Kwizera.
Bao hilo liliwafanya wachezaji wa APR kuchanganyikiwa na
kuifanya Yanga kucheza kama ipo uwanja wa nyumbani. Hadi mapumziko, Yanga ilikuwa mbele kwa bao
1-0.
APR walianza kipindi cha pili kwa kasi na kulishambulia kama
nyuki lango la Yanga, lakini mabeki
wakiongozwa na Kelvin Yondani, Vincent Bossou, Haji Mwinyi Mngwali, Pato
Ngonyani kwa kushirikiana na kipa wao, Ali Mustafa waliokoa hatari zote.
Yanga ilionekana kucheza kwa malengo zaidi katika
kipindi hicho na kulinda zaidi eneo la
kiungo chini ya wachezaji wake, Thaban
Kamusoko, Niyonzima na Deus Kaseke ambao waliwanyima wachezaji wa APR kupanga mashambulizi.
Kocha wa Yanga alifanya mabadiliko kwa kumtoa Tambwe na
nafasi yake kuchukuliwa na Simon Msuva ambaye aliongeza kasi ya mashambulizi
katika mechi hiyo ambayo ilihudhuriwa na wanajeshi kibao.
Yanga ikizinduka na kuongeza bao la pili katika dakika ya 74
kupitia kwa Kamusoko baada ya kupiga pasi zaidi ya 20 kablaya kufunga. kukiwa
kumesalia dakika 7 mpira kumalizika,
Niyonzima alitoka na nafasi yake
kuchukuliwa na Mbuyu Twite ambaye alihimarisha safu ya ulinzi.
Makosa yaliyofanywa na kipa Ali Mustafa dakika za nyongeza,
ziliizawadia goli la kufuta machozi APR kupitia kwa Patrick Sibomana. Kwa
ushindi huo, Yanga imejiweka katika
nafasi nzuri ya kusonga mbele na inahitaji sare ya aina yoyote ili kucheza
mzunguko wa pili. Mechi ya marudiano itachezwa Machi 19 kwenye uwanja wa Taifa
jijini.
Azam nao watashuka dimbani majira ya saa moja huko jijini Johanesburg kukipiga na Bidvest Wits Kombe la Shirikisho.
More
More
Referees: Bienvenu SINKO (CIV) - Mamadou Sherif BOGBE (CIV) - Kouame Gabriel KANGAH (CIV) | Stadium: Chedly Zouiten , Tunis (TUN)
More
Referees: Hamada el Moussa NAMPIANDRAZA (MAD) - Randrianarivelo RAVONIRINA HARIZO (MAD) - Augustin Gabriel HERINIRINA (MAD) | Stadium: Levy Mwanawasa , Ndola (ZAM)
More
Referees: Duncan LENGANI (MWI) - Clemence KANDUKU (MWI) - Jonizio Luwizi (MWI) | Stadium: Amahoro , Kigali (RWA)
More
Referees: Louis HAKIZIMANA (RWA) - Theogene NDAGIJIMANA (RWA) - Honoré SIMBA (RWA) | Stadium: 07 Nouvembre Rades , Rades (TUN)
More
Referees: Cecil Amatey FLEISCHER (GHA) - Malik Alidu SALIFU (GHA) - Dawood Brimah Yamdogo OUEDRAOGO (GHA) | Stadium: MODIBO KEITA , Bamako (MLI)
More
Referees: Janny SIKAZWE (ZAM) - Romeo KASENGELE (ZAM) - Oliver Gift MWEENE (ZAM) | Stadium: FNB , Johannesburg (RSA)
More
Referees: Boubou TRAORE (MLI) - Balla DIARRA (MLI) - Nouhoum BAMBA (MLI) | Stadium: Complexe Mohammed V , Casablanca (MAR)
More
Referees: Jackson Pavaza (NAM) - Matheus KANYANGA (NAM) - Isaskar BOOIS (NAM) | Stadium: Lucas 'Masterpieces' Moripe Stadium , Pretoria (RSA)
No comments:
Post a Comment