Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma (katikati) akichuana na beki wa Azam Fc, Abdallah Kheri, wakati wa mchezo wa fainali wa Kombe la Shirikisho uliopigwa jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Yanga ilishinda mabao 3-1. Kulia ni Amis Tambwe akijiandaa kutoa msaada.
**************************************************
Na Ripota wa Sufianimafoto, Dar
Mabingwa wa soka wa
Tanzania Bara, Yanga wamezidi kung’ara katika medani ya soka Tanzania baada ya
kutwaa taji la pili katika msimu wa ligi wa 2015 na 2016.
Yanga imefanikiwa kutwaa
kombe la Shirikisho la Azam Sports baada ya kuifunga timu ya Azam FC mabao 3-1
katika mchezo wa fainali uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.
Deus Kaseke (juu) akichuana na Farid Mussa.
***********************************
Ushindi huo mtamu
umeiweka timu hiyo katika chati ya juu katika sola la Tanzania na Afrika
Mashariki na Kati kutokana na ukweli kuwa imekuwa timu pekee kupata mfanikio
hayo kwa msimu huu.
Mbali ya kuwa na makombe
mawili, Yanga pia ni wawakilishi pekee katika ukanda wan chi za Cecafa kuingia
hatua ya makundi (Robo fainali) ya mashindano ya Kombe la Shirikisho Barani
Afrika.
Kipa wa Azam Fc, Aishi Manula, akipangua moja ya mpira wa hatari uliopigwa langoni kwake na Simon Msuva.
*************************************
Ushindi huo umeifanya
Yanga kupata jumla ya sh. 131 milioni. Pesa hiyo inatokana na zawadi ya Sh 50
milioni ya kutwaa kombe la Shirikisho na zawadi ya ubingwa wa Ligi Kuu ya
Tanzania Bara ya Sh 81 milioni.
Haikuwa kazi rahisi kwa
Yanga kutwaa kombe la Shirikisho kutokana na upinzani mkali wa timu ya Azam
katika mechi hiyo. Azam FC ilianza mechi hiyo kwa kasi na kulishambulia lango
la Yanga kama nyuki katika dakika za
mwanzoni na kukosa nafasi mbili za wazi, kupitia John Bocco na Mudathiri
Yahaya.
Vibweka vya mashabiki wa Yanga, mmoja wa mashabiki wa Yanga akionekana akiwa na Vyungu vinavyofuka moshi wa ubani akiwa jukwaani huku akitembea jukwaa zima wakati mechi ikiendelea.
*************************************
Yanga ilizinduka katika
dakika ya 8 na mchezaji wake, Donald Ngoma alikosa bao a wazi baada ya kupiga
shuti hafifu lililodakwa kirahisi na kipa bora wa mashindano hayo, Aishi
Manula.
Amis Tambwe akishangilia moja kati ya mabao yake mawili hiyo jana.
**********************************
Makosa yaliyofanywa na
beki chipukizi wa Azam FC, Gadiel Michael yaliipa Yanga bao la kungoza katika
dakika ya 10 kupitia kwa Amissi Tambwe aliyefunga kwa kchwa kufuatia krosi ya
mchezaji bora wa mechi hiyo, Juma Abdul.
Beki wa Yanga, Juma Abdul, akiruka kukwepa kwanja la beki wa Azam Fc, Gadiel Michael.
*************************************************
Michael alishindwa
kumzuia Abdul kupiga krosi hiyo na kumfiki Tambwe akiwa katikati ya mabeki
wawili wa Azam, Kheri Abdallah na Erasto Nyoni.
Bao hilo lilidumu mpaka
mapumziko. Azam FC ilianza kipindi cha pili kwa kufanya mabadiliko kwa kumtoa
Bocco na nafasi yake kuchukuliwa na Didier
Kavumbagu, mabadiliko ambayo yaliongeza kasi ya mchezo. Yanga ilifunga bao la
pili kupitia kwa Tambwe katika dakika ya 47 baada ya kumzidi mbio Michael na
kupiga krosi safi kwa Tambwe aliyefunga kirahisi.
Azam FC ilisawazisha
dakika moja baadaye kupitia kwa Kavumbagu baada ya kupokea pasi ya Ramadhan Singano. Bao
la tatu la Yanga lilifungwa na Deus Kaseke kufuatia gonga safi za Thabani
Kamusoko na Msuva ambaye alitengeneza mabao mawili katika mechi hiyo.
Mchezaji wa Ndanda Fc, Atupele Green, akipokea zawadi ya mfungaji bora wa mashindano hayo.
*****************************************
Rais wa TFF, Jamal
Malinzi alikabidhi medali na kombe kwa washindi wa mechi hiyo pamoja na Atupele
Green wa Ndanda FC aliyeibuka mfungaji bora kwa kufunga mabao matano. Zawadi ya
kipa Bora ilichukuliwa na Aishi Manula na mchezaji bora wa mechi ya fainali ni
Juma Abdul.
Beki wa Yanga Mwinyi Haji (kulia) akichuana na Ramadhan Singano.
Mwinyi Haji,akimfinya Erasto Nyoni....
Mwinyi Haji (kulia) akichuana kuwania mpira na Singano....
Shabiki wa Yanga, akikatiza mitaa ya Keko huku akiwa amejichora mwilini wakati akielekea Uwanjani.
Sehemu ya mashabiki wa Yanga.
Msuava akiwania mpira na Agrey
Ilikuwa ni mshike mshike.....
Ngoma, akichuana na Morris
Sehemu ya mashabiki wa Yanga.......
Azam wakiwa Live kurusha mechi hiyo....
Sehemu ya mashabiki wa Yanga, wakiwa jukwaani na mchezaji mpya wa Yanga,Hassan Kessy
Msemaji wa Yanga, Jerry Murro, akiwachangamsha mashabiki wake jukwaani
Sehemu ya Mashabiki wa Yanga....
Hassan Kessy, akiwa jukwaani akifuatilia mtanange huo....
''Nakuomba urudi timu ya Taifa'', Rais wa TFF,Jamal Malinzi akimnong'oneza beki wa Yanga Nadir Haroub 'Canavaro', wakati akisalimia benchi la Yanga.
Wachezaji wa Yanga wakipokea zawadi zao
Beki wa Yanga, Juma Abdul, akipokea zawadi yake ya kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo.
Kipa wa Azam Fc, Aishi Manula, akipokea zawadi yake ya Kipa bora wa mechi.
Juma Abdul. akipongezwa na Kocha wake baada ya kupokea zawadi.
Juma Abdul, akisalimiana na Hassan Kessy na kumkaribisha rasmi kundini na kumtambulisha kwa mashabiki wa Yanga.
Juma Abdul akizunguka na Hassan Kessy kumtambulisha kwa mashabiki....
Karibu sana dogo.....
Canavaro akisalimiana na kupeana fair play na Said Morad baada ya mchezo huo.
Warembo wakiwasilisha zawadi uwanjani baada ya mchezo huo.
Hassan Kessy, akijitambulisha kwa mashabiki wa Yanga huku akionyesha staili yake ya kupaa A.K.A Wa Kimataifa.
Kaseke akimtoka Mugilaneza....
Kaseke (katikati) akiwatoka Singano (kulia) na Nyoni


























No comments:
Post a Comment