Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana (aliyevaa sweta) akikagua maendeleo ya utengenezaji madawati kwenye karakana zinazotengeneza madawati ya wilaya za chemba na kondoa, leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana (aliyevaa sweta) akikagua maendeleo ya utengenezaji madawati kwenye karakana zinazotengeneza madawati ya wilaya za chemba na kondoa.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana (aliyevaa sweta) akikagua maendeleo ya utengenezaji madawati kwenye karakana zinazotengeneza madawati ya wilaya za chemba na kondoa.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana (aliyevaa sweta) akikagua maendeleo ya utengenezaji madawati kwenye karakana zinazotengeneza madawati ya wilaya za chemba na kondoa.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana (wa pili kutoka kulia walio kalia dawati) akikagua ubora wa madawati yanayotengenezwa na wilaya ya Chemba kwa lengo la kutekeleza agizo la Mhe. Rais la kumaliza tatizo la uhaba wa madawati
Mafundi wakiendelea na kazi ya utengenezaji madawati ya Wilaya za Chemba na Kondoa kama walivyokutwa Mei 30, 2016 wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kukagua maendeleo ya utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais la kumaliza tatizo la uhaba wa madawati.
*********************************
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Mheshimiwa Jordan Rugimbana Mei 30, 2016 amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya
kazi ya utengenezaji madawati katika Wilaya za Chemba na Kondoa.
Katika ziara yake, Mheshimiwa
Rugimbana ameonesha kuridhishwa na hatua ya utengenezaji madawati iliyofikiwa
na Wilaya ya Chemba na jitihada alizoziona zimempa imani kuwa kufikia mwishoni
mwa mwezi Juni, 2016 Chemba watakuwa wamekamilisha agizo la Mheshimiwa Rais
Magufuli la kumaliza tatizo la madawati.
Mkuu wa Wilaya ya Chemba
Mheshimiwa Ramadhan Maneno alimweleza Mkuu wa Mkoa Dodoma kuwa Wilaya hiyo ina
upungufu wa madawati 9,400 na hadi
kufikia Mei 30, 2016 tayari Chemba walikuwa wamekamilisha utengenezaji wa
madawati 5,000. Aidha, tayari wameisha kusanya vifaa ambavyo ni mbao
na bomba za chuma (Flat Bar Pipes) vinavyotosheleza kutengeneza madawati
yaliyobakia na tayari vifaa hivyo vipo kwenye karakana inayotengeneza madawati
ya chemba na kazi ya utengenezaji inaendelea.
“Pamoja
na kuwepo kwa changamoto za kukatika kwa umeme mara kwa mara, Wilaya imefanya jitihada
za kuongeza idadi ya mafundi ili washambulie kazi ya madawati yaliyobakia na
kuhakikisha inakamilika kabla ya mwisho wa mwezi Juni” aliongeza Mhe. Maneno.
Kwa upande wa Wilaya ya Kondoa,
Mheshimiwa Rugimbana amemtaka Mkuu wa Wilaya hiyo kuhakikisha kazi ya kutengeneza
madawati inafanyika kwenye kituo kimoja na Wilaya kuongeza nguvu ya kazi kwa
kuongeza idadi ya mafundi na vifaa
ikijumuisha mbao na bomba za chuma (Flat Bar Pipes).
Aidha, ametaka kazi hiyo
ifanyike hadi siku za Jumamosi na Jumapili, pia vituo vya kutengenezea madawati
viwekwe taa za umeme ili kazi ya utengenezaji ifanyike usiku na mchana kwa
utaratibu utakaofaa.
Nae Mkuu wa Wilaya ya Kondoa
Mheshimiwa Shaban Kissu ameahidi kufikia Juni 15, 2016 Kondoa itakua inamalizia
utengenezaji wa madawati yanayohitajika kwenye Wilaya hiyo kwani kwa sasa
wamenunua mbao kwa bei nafuu kutoka Wilaya ya Chemba na Bomba za Chuma (Flat
Bar Pipes) kutoka viwandani ambapo kwa pamoja vifaa hivyo vitatosha
kutengenezea madawati yaliyobakia kulingana na mahitaji.
Taarifa ya Wilaya ya Kondoa imeonesha
kuwepo kwa upungufu wa madawati 10,580 wakati
yaliyokamilika kutengenezwa hadi sasa ni madawati 2,299 na yaliyo katika hatua za mwisho za matengenezo ni madawati 1,322.
Akihitimisha ziara yake ya
ukaguzi, Mkuu wa Mkoa Dodoma Mhe. Rugimbana amezitaka Wilaya za Dodoma
kushirikiana ikiwa ni pamoja na zile Wilaya zenye misitu kuzisaidia mbao Wilaya
ambazo zina uhaba wa misitu, Wilaya zilizofanikiwa utengenezaji wa madawati
kama Chemba na Dodoma kuwapa uzoefu Wilaya zenye changamoto na kuahidi kuwa
mwishoni mwa wiki atakamilisha kufanya ziara ya ukaguzi wa madawati kwenye
Wilaya za Chamwino, Kongwa, Mpwapwa na Bahi.
Imetolewa
na:
Idara
ya Mawasiliano ya Serikali
Ofisi
ya Mkuu wa Mkoa
DODOMA
Mei 31,
2016

No comments:
Post a Comment