Habari za Punde

*AZAM FC WAANZA KUJIFUA MAKOCHA NA MAKOCHA WAHISPANIA

Na Ripota wa Mafoto Blog, Dar
KLABU ya Azam FC, wameanza mazoezi yao ya  kujiandaa na msimu ujao wa ligu Kuu Tanzania Bara (2016-17) ikiwa chini ya benchi jipya la ufundi linaloongozwa na makocha kutoka nchini Hispania, Zeben Hernandez na Msaidizi wake Yeray Romero, Kocha Mkuu wa Viungo Jonas Garcia na Msaidizi wake, Pablo Borges huku Kocha wa Makipa akiwa ni Jose Garcia na Daktari wa timu, Sergio Perez, akitarajia kutua nchini muda wowote kuanzia sasa.
Akizungumza na Mtandao huu, Mtendaji mkuu wa Azam Fc,  Saad Kawemba, alisema kuwa kwa sasa wapo kwenye mikakati ya kuongeza nguvu kwenye kikosi hicho kwa kusajili wanne wa kimataifa baada ya Didier Kvaumbagu na Allan Wanga kuondoka.  
‘’Zaidi pia tunahitaji golikipa wa kimataifa ambaye atasaidiana na Aishi Manula na ambaye  pia atakuwa msaada kwetu katika michuano ya kimataifa na katika  ligi msimu ujao ambao tunahitaji ubingwa na hilo linawezekana kwani nia tunayo,
Tunahitaji kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa na hata katika ligi pia ndiyo maana tunataka kufanya usajili utakaokuwa na manufaa kwetu na tumeonelea ni bora kutafuta kwanza golikipa wa kimataifa, beki wa kati na washambuliaji wawili wa kimataifa ambao watachukua nafasi za Kavumbagu na Allan Wanga,"amesema Kawemba.
Aidha Kawemba, alisema kuwa kwa sasa wameamua kupandisha vijana wanne kutoka timu ya vijana pia na wamefanya mchanganuo wa vikosi ambapo kwa sasa watakuwa na vikosi viwili kila kimoja kitakuwa na wachezaji 22.

Makocha hao wataongezewa nguvu na makocha wengine wazawa waliokuwepo na kikosi hicho msimu uliopita kama Kocha Msaidizi Dennis Kitambi na Idd Abubakar, aliyekuwa akiwafua makipa wa Azam FC.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.