Habari za Punde

*KIGANJA: TOC JIFUNZENI KUPITIA NCHI ZINGINE ILI KUKUZA NA KUENDELEZA MICHEZO NCHINI

 Mtendaji Mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa Bw. Mohamed Kiganja akicheza mpira wa meza na Mkufunzi wa Shirikisho la Dunia kutoka Egypty Ahmed Dawlatly baada ya ufunguzi wa mafunzo hayo katika Shule ya Msingi Kisutu leo asubuhi
  Mtendaji Mkuu wa Baraza Bw. Mohamed Kiganja akizungumza na waandishi wa habari na kutoa maelekezo kwa Viongozi wa TTTA (hawapo pichani) kuhusu kupanua wigo wa mchezo huo katika vituo vingine Mkoa wa Dar es salaam pamoja na mikoa mingine. Kushoto ni Mkufunzi wa Mpira wa Meza wa Shirikisho la mchezo huo la duninia kutoka Egypty Ahmed Dawlatly.
 Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Baraza Bw. Mohamed Kiganja hayupo pichani wakati akifungua mafunzo.
Mtendaji Mkuu wa BMT Bw. Mohamed Kiganja (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkufunzi wa Mpira wa Meza wa Shirikisho la mchezo huo la dunia kutoka Egypty Ahmed Dawlatly (kushoto), Kaimu Mwenyekiti wa TTTA Athony Mutafurwa (kulia) baada ya ufunguzi.
**************************************
Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bw. Mohamed Kiganja ameitaka Kamati ya Oliympiki Tanzania (TOC) wajiulize na kujifunza jinsi nchi zingine zinavyokuza na kuendeleza michezo kupitia  kamati hizo.
Rai hiyo ameitoa leo wakati akifungua mafunzo ya Ualimu wa Mpira wa Meza yanayofanyika kwa siku nane kuanzia tarehe 4 hadi 11 Julai mwaka huu katika Shule ya Msingi Kisutu jijini Dar es salaam.
Aidha, ameitaka Kamati hiyo kuweka wazi kwa vyama mambo wanayotakiwa kuyafanya kuendeleza michezo wanayoelekezwa na Kamati ya Olimpiki ya dunia.
“TOC jengeni mahusiano yakaribu na muwe wawazi kwa vyama, mpo kwa ajili ya kuendeleza michezo, fanyeni vile mnavyoelekezwa na Kamati hii  duniani”, alisema Kiganja.
Katika hatua nyingine Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza Bw. Mohamed Kiganja amekielekeza chama cha mchezo wa meza kupanua wigo kwa  kuanzisha vituo vingine katika Manispaa za Kinondoni na Temeke na katika shule tofauti za Mkoa wa Dar es salaam na wasitegemee kituo kimoja cha shule ya Kisutu pekee.
Aliendelea kuwa, chama hakina budi kwenda mbali zaidi katika Mikoa mingine ambapo, aliwahakikishia kuwa,   Baraza liko tayari kuwasaidia kwa Makatibu Tawala ili kuona mchezo huo unakuwa katika Mikoa yote nchini.
“Tuwatengenezee mazingira Walimu wanaopata mafunzo”, alieleza.
Awali  Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Meza (TTTA) Bw. Athony Mutafurwa ameeleza changamoto zinazokikabili chama cha mpira wa meza ni pamoja na Uwanja na fedha ambapo ameeleza kuwa, TTTA inaishauri Serikali kurudisha mfumo wa kutoa ruzuku kwa vyama na kuongeza kuwa:
Serikali ione umuhimu wa kujenga uwanja wa ndani wenye hadhi ya kimataifa katika awamu ya pili ya ujenzi wa uwanja wa Taifa ili Tanzania tuweze kuandaa mashindano ya kimataifa ambayo yamekewa yakishindikana kutokana na kukosekana kwa uwanja.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.