Habari za Punde

MKUTANO MKUU WA MWAKA WA 2019 WA CHAMA CHA WAPIMA ARDHI WAFANYIKA DAR

 Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Nicholas Mkapa, (wa pili kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Upimaji Ardhi ya Gromaps Africa Ltd, Joseph Tairo, kuhusu vifaa vya upimaji ardhi wakati alipofika kufungua Mkutano mkuu wa mwaka 2019 na Kongamano la Chama cha Wapima Ardhi Tanzania (IST) uliofanyika jijini Dar esc Salaam, leo. Kushoto ni Makamu wa Rais wa hicho, Bille Mussa. (Picha Zote na Muhidin Sufiani).
 Makamu wa Rais wa Chama hicho, Bille Mussa, akijaribu kufafanua jambo kwa Naibu Katibu Mkuu huyo.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Nicholas Mkapa, (wa tatu kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi  wa Kampuni ya Upimaji Ardhi ya Global Sarvay  Ltd, Daud Msungu, kuhusu vifaa vya upimaji ardhi wakati alipofika kufungua Mkutano mkuu wa mwaka 2019 wa Chama cha Wapima Ardhi Tanzania (IST) uliofanyika jijini Dar es Salaam, leo sambamba na Kongamano. 
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Nicholas Mkapa, (wa tatu kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja Mradi wa Kampuni ya Cosmomaps Consult Ltd, Khatibu Semkieti, kuhusu vifaa vya vinavyotumiwa na wapimaji ardhi wakati alipofika kufungua Mkutano mkuu wa mwaka 2019 wa Chama cha Wapima Ardhi Tanzania (IST) uliofanyika jijini Dar es Salaam, leo sambamba na Kongamano. 
 Mshiriki wa Kongamano hilo akipitia maandiko.
 Washiriki wakisikiliza kwa makini.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Nicholas Mkapa, akizungumza wakati akifungua Mkutano mkuu na Kongamano la mwaka 2019 la Chama cha Wapima Ardhi Tanzania (IST) uliofanyika jijini Dar esc Salaam.
********************************************************
SERIKALI kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imewataka wadau wa ardhi kutoa maoni ya sheria zilizopitwa na wakati ili ziweze kufanyiwa marekebisho mara moja.
Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Nicholas Mkapa kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wiliam Lukuvi wakati wa ufunguzi wa kongamano la wapimaji ardhi Tanzania na Mkutano Mkuu wa mwaka wa IST uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkapa alisema serikali imekuwa ikitunga sheria na kanuni ili ziweze kutoa dira ya kiutendaji  na kusimamia utendaji wa wana taaluma husika.
“Natambua kuwa taaluma ya upimaji  na ramani nchini inaongozwa  na sheria mbili  yaani CAP324 ordinance law na Sheria namba mbili ya mwaka 1977,hizi za zamani na zimepitwa na wakati hivyo zinahitaji kufanyiwa marekebisho ili ziweze kuendana na wakati,” alisema.
Alisema sasa taaluma ya upimaji imekuwa,teknolojia na uandaaji wa ramani umekuwa ukibadilika kwa kiwango kikubwa na kusababisha sheria hizo kuwa kikwazo cha maendeleo ya taaluma hiyo.
“Wizara yangu imetoa maelekezo kwa wadau wote kutoa maoni ili sheria hizo zifanyiwe marekebisho na nimemuelekeza mkurugenzi wa upimaji ramani  kuwashirikisha wadau wote kutoa maoni ili kuweza kupata sheria itakayokidhi mahitaji,matumaini yangu mchakato huu utaharakishwa ili marekebisho yafanyike mapema na kuendana na kasi ya serikali katika utekelezaji wa  majukumu yenu,”alisema.  KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Vilevile Mkapa alisema wizara hiyo kwa kushirikiana na watamu wa kimataifa imeshakamilisha kazi ya kuunda mfumo mpya wa upimaji utakaotumika kwa ajili ya kazi zote za upimaji ardhi.
 Alisema mfumo huo unaendana na unatumika kimataifa  ambao unatumia taarifa zilizoboreshwa kuhusu ukubwa na umbo la dunia.
Mkapa alisema mfumo huo umekamilika na unatarajiwa mwishoni mwa mwaka  kuchapishwa kwenye gazeti la serikali.
Pia ameitaka IST kuweka mkakati maalumu wa kujenga utaratibu wa kudhibiti maovu  kwa taaluma hiyo  ili kuweza kutoa ushirikiano wa kutosha kwa serikali na kutoa msaada wa ufafanuzi wa mwenendo wa taaluma  na watalamu wa upimaji.  
RAIS WA IST
 Makamu wa Rais wa Chama cha Wapimaji Ardhi Tanzania, Bille Mussa, akizungumza katika mkutano huo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua rasmi.
Naye Rais wa Chama cha Wapimaji Ardhi Nchini(IST) Bille Mussa alisema mkutano huo umewakutanisha wataalamu wa upimaji ardhi 130 na kampuni tano ambazo mbili zimefadhili mkutano na tatu zimeshiriki maonesho.
 Alisema lendo la mkutano huo ni kukidhi matakwa ya kikatiba ya chama hicho,kujadili changamoto  za kitaalamu na kuangalia muelekeo wa taaluma ili kujenga uwezo juu ya teknolojia inayobadilika kila siku.
Mussa alisema mkutano huo umebebwa na kauli mbiu ya upimaji ardhi na maendeleo endelevu katika sekta ya ardhi mafanikio na changamoto zake.
Hata hivyo aliiombna wizara hiyoi kuharakisha marekebisho ya sheria zilizopitwa na wakati  na kuendeleza ushirikiano uliopo kwa manufaa ya watanzania.
WADAU WANENA
Naye mwalimu wa Upimaji wa Ardhi, Joseph Tairo alitaja changamoto inayoikumba taaluma hiyo ni ajira hivyo aliiomba wizara kuangalia  namba ya kuweza kuwaajiri wanataaluma kwani wanahitajika sana kwa maendeleo ya taifa.
“Kikubwa wapimaji ardhi waajiriwe  kwani wengi wao wamemaliza masomo na kufanya kazi kwenye taasisi au kampuni tofauti na walichokisomea,hivyo ni vyema mfumo wa ajira ukaangaliwa kwa namna yake,”alisema.

Naye Mpima Ardhi Kanda ya Kaskazini,Nina Rutakyamirwa ambaye ni ambaye alikuwa mwanamke wa kwanza kwenye taaluma hiyo mwaka1992,aliwahimiza wanawake kutoiogopa fani hiyo kwani haina toifauti na  ya uhandisi. 
 Mkono wa pongezi kwa wadau
 Mkono wa pongezi kwa wadau
 Mkono wa pongezi kwa wadau 
  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Nicholas Mkapa, (katikati) akimkabidhi cheti cha shukrani Mpimaji Ardhi Godwin Saiguran, wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka 2019 na Kongamano la Chama cha Wapima Ardhi Tanzania (IST) uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Nicholas Mkapa, (wa pili kushoto) akimkabidhi cheti cha shukrani Mpimaji Ardhi wa Chuo cha Madini Dodoma, Sunday Brown, wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka 2019 na Kongamano la Chama cha Wapima Ardhi Tanzania (IST) uliofanyika jijini Dar es Salaam,
 Cheti cha shukrani 
 Picha ya pamoja
 Picha ya pamoja
Ujumbe maalumu.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.