Wachezaji wa timu ya Taifa wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wa Ur 11
Mchezaji wa Timu ya Taifa Taifa Stars, Simon Msuva, akicheza soka na watoto umri chini ya miaka 11 wa kituo cha Karume Academy wakati timu ya Taifa ilipotembelea Kliniki ya watoto 'Youth Soccer Clinic' iliyoratibiwa na Afrisoccer kwa ushirikiano na Shirikisho la Soka Tanzania TFF, iliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Kimataifa ya Laureate iliyopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, leo. (Picha na Muhidin Sufiani).
Mchezaji wa Timu ya Taifa Taifa Stars, Iddi Seleman, akicheza soka na watoto umri chini ya miaka 11 wa kituo cha Karume Academy wakati timu ya Taifa ilipotembelea Kliniki ya watoto 'Youth Soccer Clinic' iliyoratibiwa na Afrisoccer kwa ushirikiano na Shirikisho la Soka Tanzania TFF, iliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Kimataifa ya Laureate iliyopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.
Watoto wakijaribu kuonyesha vipaji vyao
******************************************
Na Dina
Mgana
TIMU ya
Taifa ya Tanzania Taifa Stars inayotarajia
kushuka dimbani keshokutwa katika mchezo wa kufuzu Afcon 2021, leo imetembelea
Kliniki ya watoto wachezaji iliyoandaliwa
na AfriSoccer kwa ushirikiano na
Shirikisho la Soka Tanzania TFF, katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya ‘Laureate
International’ iliyopo Mbezi Beach
Jijini Dar es salaam.
Katika ziara
hiyo wachezaji hao walipata fursa ya kuzungumza na watoto hao na kucheza pamoja
huku wakiwaasa kupenda michezo na kuzingatia masomo ili waweze kufikia malengo
yao yao ya kimichezo.
Akizungumza
katika ziara hiyo Nahodha wa timu yatifa, Mbwana Samatta, aliwapongeza
waandaaji wa Kliniki hiyo kwa kuweza kuwakusanya watoto na kuwapa elimu ya Soka
na kuwakutanisha na wachezji wa timu ya Taifa ili kuwapa hamasa.
‘’Hata sisi
pia tulikuwa kama ninyi na tulikuwa na ndoto za kufika hapa tulipo kwa sasa
lakini njia pekee ni kufuata maelekezo ya walimu wenu wa michezo na shuleni,
kuzingatia ratiba ya mazoezi na kutojihusisha na makundi yasiyofaa’’. Amesema
Samatta.
Kliniki hiyo
imehusisha watoto wa Kituo cha TFF na Shule ya Sekondari ya Laureate ambapo
waliweza kucheza mechi pamoja na michezo mingine.
Mchezaji wa Timu ya Taifa Taifa Stars, Simon Msuva, akicheza soka na watoto umri chini ya miaka 11 wa kituo cha Karume Academy wakati timu ya Taifa ilipotembelea Kliniki ya watoto 'Youth Soccer Clinic' iliyoratibiwa na Afrisoccer kwa ushirikiano na Shirikisho la Soka Tanzania TFF, iliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Kimataifa ya Laureate iliyopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, leo.
Nahodha wa timu ya taifa Mbwana Samatta, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto.
Kipa wa timu ya Taifa, Juma Kaseja akiwafundisha makipa watoto
Picha ya pamoja.
No comments:
Post a Comment