Rais Mstaafu awamu ya Pili Alhaji Hassan Mwinyi akitoa salamu zake kwa wageni waalikwa wakati wa sherehe yake ya kuzaliwa ambapo jana alitimiza umri wa miaka 90.Sherehe hiyo ilifanyika katika hoteli ya Sea Cliff na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Rais Mstaafu awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi kwa kutimiza miaka 90 wakati wa sherehe ya kuzaliwa kwake iliyofanyika katika hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkewe Mama Siti Mwinyi.
No comments:
Post a Comment