Mratibu wa B Ball Kitaa Karabani Karabani inayodhaminiwa
na kinywaji cha Sprite akizungumza na waandishi wa habarileo jijini Dar-es-Salaam kuhusu mechi
ya mpira wa kikapu utakaochezwa siku ya ijumaa Juni 5 wiki hii katika
uwanja wa BBK Park. Kulia ni nahodha wa
timu ya East Zone 2 Haby Mayeye.
Michuano ya Bball Kitaa ngazi ya kanda
inayodhaminiwa na kinywaji cha Srite, mwaka huu inatarajiwa kuzinduliwa jijini
Dar es Salaam Ijumaa wiki hii, ambapo kutakuwa na pambano kali
litakalozikutanisha timu kutoka kanda ya kwanza ya mashariki ambayo inaundwa na wachezaji kutoka Msasani,
Oysterbay na Masaki dhidi ya timu kutoka kanda ya pili ya magharibi ambayo
inaundwa na wachezaji kutoka Mbezi Beach, Kunduchi naTegeta.
Pambano hilo ambalo linatarajiwa
kuvuta hisia za ,maelfu ya mashabiki kutoka wilaya zote za jiji la Dar es
Salaam yaani Kinondoni, Temeke na Ilala litafanyika katika uwanja wa Bball
Kitaa Park,uliopo karibu na ukumbi maarufu wa Gymkhana jijini Dar es Salaam.
“Lengo kuu la mechi hii ni kuwafanya
mashabiki wote wa kujumuika katika michuano hii mikubwa kabisa ya Bball Kitaa
ngazi ya kanda, ambayo inatarajiwa kuanza Julai na kuzikutanisha kanda zote
mbili za jiji la Dar es Salaam,” Karabani ambaye ni mratibu wa Bball Kitaa aliwaambia
waandishi.
Karabani pia alizitaja kanda zingine
ambazo zitashiriki katika michuano hiyo mwezi Julai kuwa, ni mabingwa watetezi
Kanda ya Nne ya Mashariki inayoundwa na wachezaji kutoka Temeke na Mbagala, Kanda
ya Kwanza ya Mashariki, Kanda ya Tatu ya Mashariki, Kanda ya Pili ya Magharibi,
Kanda ya Tatu ya Magharibi na Kanda ya Kanda ya Nne ya Magharibi. Mshindi wa
michuano hii ya nne ngazi ya kanda atakabidhiwa
kitita taslimu cha shilingi za Kitanzania milioni 5.
Kwa
upande wake, Meneja bidhaa wa Coca-Cola nchini Maurice Njowoka alisema kuwa kampuni ya
Coca-Cola imejiona ni yenye heshima kubwa mara baada ya kupewa fursa ya
kudhamini michuano hiyo nchini na kuahidi kuwa kampuni yake kuendelea kutoa
ushirikiano wa bega kwa bega kuhakikisha kuwa mchezo huu unazidi kusonga mbele.
“Sote
tunafahamu kuwa mchezo wa mpira wa kikapu ni mojaya michezo yenye mashabiki
wengi sana nchini hasa kwa vijana ambao wanahitaji fursa hii adhimu ili
kuendeleza vipaji vyao na kutimiza ndoto zao pia”, alisema Njowoka.
Michuano ya Bball Kitaa ambayo kwa
takribani miaka miwili sasa imekuwa ikifanyika nchini, imejikita katika kujenga
misingi imara ya maisha na kuwaburudisha vijana na hivi karibuni Chama Cha
Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (RBA), kimekuwa kikiitumia michuano hii
kama moja ya njia za kupata vipaji vipya nchini.
“Nina furaha sana kuona Bball Kitaa
sasa inatambuliwa na Chama cha Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (RBA) na
sote tunaamini kuwa ushirikiano huu utazidi kadiri siku zinavyokwenda ili
kuendeleza mchezo huu hapa nchini”, Karabani alisema huku akizidi kumimina
shukrani zake za dhati kwa Sprite kwa
moyo wao katika kuhakikisha Bball Kitaa inazidi kusonga mbele.
No comments:
Post a Comment