Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga ya jijini Dar es Salaam na JKT Ruvu, umemalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa, huku wakiibuka na ushindi wa mabao 4-1. Mabao ya Yanga yalifungwa na Donald Ngoma katika dakika ya 30, Amis Tambwe dakika ya 48 na 60, Thaban Kamusoko, dakika ya 87. Bao la kufutia machozi la JKT Rubu lilifungwa na Naftali Nashon katika dakika ya 50.
Huko katika viwanja vingine, MBEYA CITY 0- TANZANIA PRISONS 1- Uwanja wa Sokoine Mbeya
STAND UNITED 2- AFRICAN STARS 0 Uwanja wa Kambarage, Shinyanga
MGAMBO JKT 2- MAJIMAJI 0 - Uwanja wa Mkwakwani
Thaban Kamusoko, akipongezwa na kocha wake baada ya kufunga bao la nne, katika dakika ya 87
Simon Msuva wa Yanga, akiruka daruga la beki wa JKT Ruvu, Madenge Ramadhan
Kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima (kushoto) akimenyana na beki wa JKT Ruvu, Napho Zuber
Beki wa JKT akiruka kuokoa hatari
Mshambuliaji wa Yanga, Godfrey Mwashiuya, akiruka kukwepa kwanja la beki wa JKT Ruvu, Madenge Ramadhan
Msuva wa Yanga (kulia) na beki wa JKT Ruvu wakiwania mpira
Mshambuliaji wa Yanga, Godfrey Mwashiuya, akiwakimbiza mabeki wa JKT Ruvu.
Kipa wa JKT Ruvu, Tony Kavishe, akigagaa chini huku akiuangalia mpira ukitinga wavuni, na kufungwa bao la Nne lililofungwa na Thaban Kamusoko katika dakika ya 87.
Kocha wa Yanga, akitoa maelekezo kwa Nahodha wake, Nadir Haroub 'Canavaro'.
No comments:
Post a Comment