Habari za Punde

NMB YATOA MSAADA WA MATIBABU KWA WTOTO 80 WENYE VICHWA VIKUBWA NA MGONGO WAZI

Mkuu wa Idara ya Mahusiano na Mashirikiano 'Cooparate Suppot' Benki ya NMB, Valence Mtongole, akizungumza wakati wa Hafla ya kukabidhi msaada wa Kadi 80 za matibabu ya watoto wenye Vichwa vikubwa na Mgongo wazi, iliyofanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam, leo kuelekea Maadhimisho ya Kilele cha Mtoto mwenye Kichwa Kikubwa na na Mgongo wazi yatakayofanyika Kitaifa Mkoani Tanga Oktoba 25 mwaka huu.  (Picha Zote na Muhidin Sufiani).
Mratibu wa Chama cha Wazazi wenye Watoto wenye Kichwa kikubwa na Mgongo wazi ASBAHT, Hidaya Alawi, akitoa mada kwa wazazi na wadau mbalimbali wakati wa Hafla ya kukabidhi msaada wa Kadi 80 za matibabu ya watoto wenye Vichwa vikubwa na Mgongo wazi, iliyofanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam, leo kuelekea Maadhimisho ya Kilele cha Mtoto mwenye Kichwa Kikubwa na na Mgongo wazi yatakayofanyika Kitaifa Mkoani Tanga Oktoba 25 mwaka huu.
Baadhi ya wafanyakazi wa NMB na wazazi wa watoto hao wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa mbele yao.
Majadiliano kati ya wazazi na wafanyakazi wa NMB
Majadiliano yakiendelea
Wafanyakazi wa NMB wakiwa katika picha ya pamoja baada ya hafla hiyo
Baadhi ya wafanyakazi wa NMB wakiwa katika picha ya pamoja na wazazi wenye watoto wenye vichwa vikubwa.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.