Habari za Punde

*ALIYENENEPESHA NYETI AANZA KUTIBIWA INDIA

Na Herrieth Benny, jijini Dar es Salaam

ALIYENENEPESHA nyeti hadi kufikia zaidi ya kg10 , Gasper Honza tayari amenza kupatiwa matibabu Nchini India.
Jopo la madaktari wa hospitali hiyo (jina tunalo) tayari wameanza kufanya uchunguzi wa awali kwa kuchukua kipande cha nyama kutoka kwenye nyeti zake ili kubaini kemikali zilizokuwamo kwenye dawa aliyotumia.
Akizungumza na Sufianimafoto kwa njia ya simu jana kuhusiana na matibabu hayo, Gasper alisema tayari jopo hilo limempa dawa ya kupaka aina ya Hip absorb kwa ajili ya kupunguza uvimbe alionao kabla ya kumfanyia upasuaji katika nyeti yake.
“Kwa kweli tangu nimeanza kutumia dawa hii ninaona uvimbe unapungua japo napata haja ndogo chafu pamoja na maumivu makali, sina wasiwasi kwasababu nataka kupona hata hivyo daktaria wangu ameniambia nitapoteza nguvu za kiume jambo ambalo naona ni kawaida maadamu niutue mzigo huu,”alisema.
Kwa mujibu wa Dk. Hich Yagien wa India, Honza atapoteza uwezo wa nguvu za kiume baada ya upasuaji huo kutokana na uvimbe huo mkubwa kukaa kwa muda mrefu.
“Honza alifanya tofauti sana kwani dawa aliyotumia kwani dawa hiyo ni kwa ajili ya kukuza makalio ambayo zaidi hutumiwa na baadhi ya wanawake ingawa wengine waliotumia wameathirika na saratani na baadhi wamepoteza maisha baada ya upasuaji kutokana na kutokwa na damu nyingi. alisema daktari huyo
Dawa hiyo ina nguvu sana na kwa mujibu wa maelezo ya dawa yenyewe mtu anatakiwa atumie mara mbili kwa wiki, lakini mtu anapoitumia bila kufuata masharti matokeo yake ni kama hayo ya kuvimba nyeti ama makalio bila mpngilio. ” alisema Dk. Yagien.
Alisema Honza atafanyiwa upasuaji mara baada ya vipimo kukamilika mwishoni mwa wiki hii.
Aidha alisema kuwa Honza si mgonjwa wa kwanza kukutana naye kwani ameshakutana na wagonjwa wa aina hiyo wengi tu ambao ameshawatibia kwa kuwafanyika upasuaji huku wengine wakifikishwa hospitalini hapo wakiwa wameoza.
Honza ambaye ni Mkazi wa Mbezi Beach Dar es Salaam, anatarajia kufanyiwa upasuaji huo wiki ijayo baada ya kutumia dawa ya kukuza makalio aina hypson akiwa na nia ya kukuza Nyeti ili kuinusuru ndoa yake Septemba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.