imemteua Mbunge wake wa jimbo la Mbulu, Mustapha Akonay, kuwania unaibu spika.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, John Chiligati, alisema kuwa, mkutano wa Kamati ya Wabunge wa CCM imempa ushindi wa kishindo Ndugai, aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge lililopita.
Akizungumza na waandishi wa habari, Chiligati alisema hadi jana jioni, wanachama watatu wa CCM walijitokeza kuwania nafasi hiyo, ambao ni Ndugai, Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama na Mbunge wa Magu, Dk. Festus Limbu.
Alisema wakati wa mkutano jana, Dk. Limbu alitangaza kuondoa jina lake kwenye kinyang’anyiro hicho, akisema hana sifa kama walizonazo wagombea wenzake.
Kwa mujibu wa Chiligati, Jenista, aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge lililopita alipokuwa akijieleza mbele ya wagombea, alisema anaondoa jina lake, hivyo asipigiwe kura.
No comments:
Post a Comment