Hongera Mrembo Jacqueline kwa kutimiza miaka 25 sasa tangu kuzaliwa kwako mungu akuzidishie heri na uzima na moyo wa kuwakumbuka Yatima kama hivi. Na hii ndiyo Keki ya mrembo huyo inayosubiri kukatwa rasmi leo jioni.
Jacqueline, akipozi kwa picha ya kumbukumbu na baadhi ya Watotot yatima wa Kituo cha New Life Orphans Home, wakati alipowatembelea watoto hao na kucheza nao na kufurahi kwa pamoja, ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Siku yake ya kuzaliwa.
Ilikuwa ni furaha kwa watoto hao na mrembo huyo mpenda watoto, kwani baby huyu aliyebebwa hakutaka hata kushuka wakati alipokuwa akiwaaga kuondoka mahala hapo kwa jinsi alivyojihisi furaha kwa wakati huo, ama hakika ilikuwa kazi kubwa kumwacha mtoto huyu na kuondoka.
No comments:
Post a Comment