Na Mwandishi wa Sufianimafoto
SHINDANO la kusaka vipaji vya waimbaji wa
muziki wa dansi nchini,kuanza Desemba 20 na
kukamilika mwezi wa tatu mwakani.
Shindano hilo lililoandaliwa maalum kwa ajili
ya kutafuta na kuibua vipaji vya vijana wenye
uwezo wa kuimba aina hiyo ya muziki, pia
linamalengo ya kukuza vipaji vya wasanii hao
ambao wengi wamekuwa wakishinda jinsi ya
kuibuka na kujitambulisha katika jukwaa la
muziki wa dansi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar
es Salaam jana, Mkurugenzi wa Makwekwe
Entertainment, Suleiman Mathew, alisema kuwa
katika shindano hilo, vikundi mbalimbali
vitachuana kuwania taji la kundi bora nchini.
“Tumeona tushiriki kukuza na kuendeleza
vipaji vya vijana wetu, kwa kupitia muziki wa
dansi nchini, muziki ambao unakimbiwa na
vijana wengi ambao hukimbilia katika Bongo
Fleva", alisema Mathew.
Aidha alitaja ratiba ya mchakato huo kuwa, Desemba 20 na 21 saa 4 hadi saa 10 za jioni,
usaili wa wanamuziki hao utafanyika Rufita
Baa, Sinza Mori katika Wilaya ya Kinondoni, Na
Ilala wao utafanyika katika Ukumbi wa DDC
Kariakoo, Desemba 23 na 24 muda ule ule, huku
Temeke ukifanyika katika Ukumbi wa Ikweta
desemba 27-28.
muziki wa dansi nchini,kuanza Desemba 20 na
kukamilika mwezi wa tatu mwakani.
Shindano hilo lililoandaliwa maalum kwa ajili
ya kutafuta na kuibua vipaji vya vijana wenye
uwezo wa kuimba aina hiyo ya muziki, pia
linamalengo ya kukuza vipaji vya wasanii hao
ambao wengi wamekuwa wakishinda jinsi ya
kuibuka na kujitambulisha katika jukwaa la
muziki wa dansi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar
es Salaam jana, Mkurugenzi wa Makwekwe
Entertainment, Suleiman Mathew, alisema kuwa
katika shindano hilo, vikundi mbalimbali
vitachuana kuwania taji la kundi bora nchini.
“Tumeona tushiriki kukuza na kuendeleza
vipaji vya vijana wetu, kwa kupitia muziki wa
dansi nchini, muziki ambao unakimbiwa na
vijana wengi ambao hukimbilia katika Bongo
Fleva", alisema Mathew.
Aidha alitaja ratiba ya mchakato huo kuwa, Desemba 20 na 21 saa 4 hadi saa 10 za jioni,
usaili wa wanamuziki hao utafanyika Rufita
Baa, Sinza Mori katika Wilaya ya Kinondoni, Na
Ilala wao utafanyika katika Ukumbi wa DDC
Kariakoo, Desemba 23 na 24 muda ule ule, huku
Temeke ukifanyika katika Ukumbi wa Ikweta
desemba 27-28.
No comments:
Post a Comment