Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri mkuu Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi ,akizungumza na waandishi wa habari na baadhi ya maofisa wa Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya Nchini baada ya kuitembelea Tume hiyo ijini Dar es Salaam leo. Pamoja na mambo mengine amesema kuwa tume hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ile ya kuthibiti uingizwaji wa biashara haramu ya dawa za kulevya pamoja na udhaifu wa sheria iliyopo ya kupambana na kuthibiti dawa hizo ambapo amesema kuwa Serikali imeanza mkakati wa kuunda timu itakayotoa mapendekezo kuhusu uimarishaji wa sera, muundo na urekebishaji wa sheria ya kudhibiti dawa za kulevya ya mwaka 1995, ili kutoa uwezo kwa Tume hiyo kuwashughulikia moja kwa moja wanaojihusisha na biashara hiyo. Picha Zote na Aron Msigwa- MAELEZO
Rais Dkt. Samia awasili Jijini Moscow nchini Urusi kwa ajili ya Ziara ya
Kitaifa.
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa
amesimama wakati akipokea heshima ya wimbo wa Taifa mara baada ya kuwasili
...
11 hours ago
No comments:
Post a Comment