Habari za Punde

*AZAM KUZIPIKU YANGA NA SIMBA? YAICHAPA JKT RUVU 2-0

Mrisho Ngasa wa Azam Fc (kulia) akijaribu kuuwahi mpira ili kupiga krosi, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, baina yao na JKT Ruvu uliochezwa leo jioni kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Azam imeshinda mabao 2-0. Kwa ushindi huo sasa Azama imefikisha jumla ya Pointi 35 sawa na Yanga, ambapo Azam inasaidiwa na magoli mengi ya kufunga na machache ya kufungwa, na Simba ikishikilia nafasi ya tatu ikiwa na Point 34. Kati ya Yanga Azam na Simba ni timu ipi itachukua ubingwa wa Tanzania Bara msimu huu? wote tusubiri kuona hadi mwisho wa Ligi.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.