

TIMU ya Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo Fleva Fc, leo jioni imeweza kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, dhidi ya wapinzania wao Bongomuvi Fc, katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Timu hizo baada ya kutambina kwa siku kadhaa huku kila timu ikitamba kuibuka na ushindi katika mchezo huo uliokuwa maalum kwa ajili ya kuchangisha fedha za kuwasaidia waathirika wa mabomu wa Gongolamboto.
Mabao ya ushindi ya timu ya Bongo Fleva yalitiwa kimiani na Msanii H-Baba.





No comments:
Post a Comment