Habari za Punde

*BREAKING NEEEWZ, WANACHUO UDSM WAPIGWA MABOMU

Askari wa kutuliza ghasia (FFU) wakifyatua mabomu ili kuwatawanya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, waliokuwa wakiandamana leo asubuhi kuelekea Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ajili ya kufikisha malalamiko yao ya posho ya Sh 5,000/ ambayo wanadai ni ndogo haitoshi kwa matumizi na badala yake wanaishinikiza Serikali kuwapa Sh. 10,000/=. Hata hivyo maandamano hayo yaliishia maeneo ya Savei baada ya kukuta ukuta wa polisi hao umetanda Barabarani huku wakitoa matangazo ya kusitisha maandamano hayo na kutawanyika, baada ya kutoa matangazo hayo na wanafunzi hao waliendelea kuwa maeneo hayo huku wakiimba ndipo askari hao waliamuliwa kuanza kufyatua mabomu ili kuwatawanya. Katika tukio hilo hakuna aliyejeruhiwa ila ni wanafunzi wachache tu waliokamatwa.
Bomu la machozi limeshaachiwa hapa likianza kufyatuka...
Wanafunzi hao wakitawanyika kwa kukimbia kila mtu na njia yake baada ya mabomu kuanza kufyatuliwa.
Wanafunzi hao wakiandamana, kutoka chuoni...
Wakiwa na mabango yao yenye ujumbe kuhusu kile wanachodai na wasichohitaji.
Safari ilikuwa ni ndefu huku wakitembe, kukimbia na kuimba ili kuifanya safari hiyo kuwa fupi zaid lakini waaapi, iliishia karibu zaidi.
Maandamano bado yalikuwa yakiendelea kutokea chuoni hapo.
Mkusanyiko ulianza kama hivi...








No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.