Habari za Punde

*TASWA KUCHAGUA MCHEZAJI BORA WA MWAKA 2010, MEI 6

SHEREHE za utoaji tuzo za wanamichezo bora wa Tanzania kwa mwaka 2010, zinazotolewa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) zinatarajia kufanyika Mei 6 mwaka huu.

Sherehe hizo zinatarajia kufanyika katika ukumbi wa NSSF Waterfront, Dar es Salaam, ambapo zitaambatana na kutangazwa kwa Mwanamichezo Bora wa Tanzania wa mwaka 2010.


Akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Ofisi za Shirikisho la Soka nchini TFF, Katibu mkuu wa Taswa Amri Muhando, alisema kuwa kamati ya utendaji ya chama hicho imeteuwa Kamati ya watu 17 ya kusimamia mchakato wa kuwapata washindi hao wa kila mchezo kulingana na vyama vilivyotuma mapendekezo na majina yao na kisha kamati itachagua Mwanamichezo Bora wa Tanzania miongoni mwa washindi hao.


“Kamati hiyo itahusisha watu 15 ambao hawahusiki na TASWA na wawili kutoka TASWA kwa ajili ya kusimamia mchakato huo wa tuzo hizo, ambapo TASWA yenyewe itabaki na jukumu la kuandaa sherehe ya tuzo,”alisema.


Amir, alisema kuwa lengo kubwa la kuunda kamati hiyo ikiwa ni kuwashirikisha kwa pamoja wadau na kuifanya tuzo iliyo bora zaidi.



Orodha kamili ya wanaounda kamati ni kama ifuatavyo.


1.Amour Hassan-Mhariri Nipashe


2. Rashid Zahoro-Mhariri Mzalendo


3. Alex Luambano-Clouds FM


4. Tulo Chambo-Mhariri Tanzania Daima


5. Muhidin Michuzi-Daily News


6. Chacha Maginga-TBC1


7.Frank Sanga-Mhariri Mwanaspoti


8.Saleh Ally-Mhariri Kiongozi Championi


9. James Range-Star TV


10.Editha Mayemba-Radio Tumaini


11. Said Kilumanga-Chanel Ten/Magic Radio


12.Rehule Nyaulawa-Mkurugenzi Times FM


13. Angel Akilimali-Meneja Vipindi Radio Uhuru


14. Masoud Sanan-Mhariri Spotistarehe


15. Amir Mhando-Katibu Mkuu TASWA


16. Alfred Lucas-Mjumbe TASWA


17.Patrick Nyembela-EATV


18: Juliana Yassoda-Naibu Mkurugenzi Idara ya Michezo


No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.