Habari za Punde

*WAMACHINGA WA MJINI SONGEA WATAKIWA KUZINGATIA KANUNI ZA USAFI WA MAZINGIRA

Waziri wa Nchi ,Ofisi ya makamu wa Rais Mazingira Dkt. Terezya Huvisa, akimwagiza mfanya biashara ndogondogo (aliyeshika mfuko) aliyekuwa amepanga bidha zake kandokando ya barabara mjini Songea kuziondoa na kuelekea maeneo waliyopangiwa na Manispaa hiyo. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Diwani wa kata ya Matogoro , Songea Bw. Charles Muhagama na Meya wa Manispaa ya Songea Bw. Ally Manya. Picha na Aron Msingwa-Maelezo

Waziri wa Nchi ,Ofisi ya makamu wa Rais Mazingira Dkt. Terezya Huvisa (katikati) akizungumza na wafanyabiashara wadogondogo (wamachinga) waliokuwa wakifanya biashara katika maeneo yasiyoruhusiwa katika manispaa ya Songea na kusababisha uchafuzi wa mazingira.

Baadhi ya wafanyabiashara wakiitii agizo la Waziri wa Nchi ,Ofisi ya makamu wa Rais Mazingira Dkt. Terezya Huvisa (hayupo pichani) la kuwataka kuondoa bidhaa zao katika maeneo ya barabara mjini Songea. Hata hivyo waliutupia lawama uongozi wa manispaa hiyo kwa kuwatoza ushuru kila siku hali iliyosababisha waendelee kufanya biashara katika maeneo hayo.

Wafanyabiashara hao waliotii amri wakihama katika eneo hilo.




No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.