Habari za Punde

*T.P. MAZEMBE WAWASILI DAR KUKIPIGA NA SIMBA MCHEZO WA MARUDIANO

Wachezaji wa timu ya T.P. Mazembe ya Kongo, wakiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jioni hii kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa marudiano na Simba, mchezo unaotarajia kuchezwa siku ya Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Baadhi ya wachezaji hao wakiwa katika Gari waliloandaliwa na wenyeji wao baada ya kuwasili. Timu hiyo baada ya kuwasili iligoma kupanda gari lililoandaliwa na Uongozi wa TFF na kudai kuwa tayari walishaandaliwa usafiri na wenyeji wao waliokuwa na Coaster mbili ambapo moja ilibeba wachezaji na moja Viongozi wa timu hiyo na kuliacha basi kubwa lililoletwa uwanjani hapo kwa ajili yao likiondoka tupu.
Baadhi ya mashabiki wa T.P Mazembe wakiimba na kucheza uwanjani hapo misebene wakati wakiisubiri timu hiyo kuwasili. kwa kweli ilikuwa ni burudani tosha kama ungebahatika kuwaona wakongoman hao jinsi walivyokuwa akizungusha miuno kwa misebene.
Hapa ni sebene tu na kuimba minyimbo ya kuwabeza wapinzani wao Simba.
Si unacheki hapa kila mmoja akizungusha....

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.