Mkazi wa Kitongoji cha Kinyenze, Mary Nathan akipita katika njia ndogo iliyofunguliwa na mwekezaji raia wa kigeni anayemiliki ardhi katika eneo la kitongoji hicho kilichopo Kijiji cha Kipera Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro.
Mwekezaji huyo analalamikiwa na wakazi wa kijiji hicho kufunga njia na kuvamia mashamba ya wakazi hao.
Wakazi hao bado wanalalamikia kufungwa kwa njia hiyo licha ya kufunguliwa lakini imetengenezwa kama ya kupitisha mifugo kwani ni nyembamba na hairuhusiwi kupitisha gari wala pikipiki jambo ambalo bado ni kero kubwa kwa wakazi hao. Picha na Mroki Mroki
Mkazi wa Kitongoji cha Kinyenze, Nuru James akipita katika njia ndogo iliyofunguliwa na mwekezaji raia wa kigeni alinayemiliki ardhi katika eneo la kitongoji hicho kilichopo Kijiji cha Kipera Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro.
No comments:
Post a Comment