
Kutokana na tatizo hilo wananchi wamemwomba mbunge wao, mchungaji Peter Simon Msigwa kuweza kuingilia kati na ikiwezekana kuandamana kama walivyowahi kufanya wananchi wa jimbo la Ubungo na mbunge wao Jonh Nyika, hadi ofisi za idara ya maji ili kusaidiwa kero hiyo.
Wamesema kuwa tatizo la maji katika eneo hilo limeendelea kuwasumbua na baadhi wamekuwa wakilazimika kutafuta maji hayo katika mifereji ya maji machafu kwa ajili ya matumizi na kuhoji ukimya wa mamlaka ya maji safi na maji taka katika manispaa ya Iringa (IRUWASA) kuendelea kuwatesa wananchi hao bila ya kutoa matangazo yoyote juu ya tatizo hilo. Imeandikwa na Francis Godwin Iringa
No comments:
Post a Comment