Habari za Punde

*HIVI ULE MPANGO WA KUVIZUIA VIBAJAJI KUINGIA KATIKATI YA MJI UMEISHIA WAPI?

Wahusika wamechemka nini kuvidhibiti Vibajaji kujazana maeneo ya katikati ya mji? Japo wahusika walianza kwa kazi na kutangaza utaratibu wa usafiri kama huu ikiwa ni pamoja na Vidaladala Hice kutofika maeneo ya katikati ya mji lakini hivi sasa inaonekana kulegeza kamba kama si kushindwa udhibiti huo kwani siku hizi imekuwa ni kawaida tu kuviona vibajaji na Pikipiki 'Bodaboda' zikiwa zimetega maeneo ya Posta Mpya pembeni mwa Jengo la Benjamin Mkapa mida ya kuanzia saa 10 jioni zikisubiri abiria.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.