Habari za Punde

*KONGAMANO LA KUJADILI RASIMU YA SERA YA MANUNUZI YA UMMA LAFANYIKA DAR

Kamishna wa  Idara ya Sera ya manunuzi ya Umma, kutoka Wizara ya Fedha Dk. Frederick Mwakibinga (kulia) akizungumza jambo na mjumbe wa kamati ya sera ya manunuzi,  Clemence Tesha, wakati wa kongamano la kujadili rasimu ya sera ya manunuzi ya umma lililofanyoka jana jijini Dar es Salaam leo. Kongamano hilo la siku moja lilihudhuliwa na wajumbe mbalimbali kutoka ofisi za Serikali na Taasisi binafsi.
Emmanuel Maliganya ambaye ni Afisa Ugavi kutoka Benki Kuu ya Tanzania  akichangia mada kuhusu utendaji  kazi wa maafisa ugavi wakati wa kongamano la kujadili rasimu ya sera ya manunuzi ya umma lililofanyoka jana jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo la siku moja liliandaliwa na Idara ya Sera ya manunuzi ya umma kuhudhuliwa na wajumbe mbalimbali kutoka ofisi za Serikali na Taasisi binafsi.
Juma Fimbo kutoka Umoja wa wataalamu wa Manunuzi na Ugavi  Tanzania akielezea jinsi maafisa ugavi wanavyotakiwa kufanya kazi zao kwa kutumia taaluma ya uchumi wakati wa kongamano la kujadili rasimu ya sera ya manunuzi ya umma.
Mkurugenzi wa Ugavi kutoka  Akaunti ya Changamoto za Milinia (Millenium Challange Account) Marieth Ngaida akichangia mada wakati wa kongamano hilo.
Kamishna wa  Idara ya Sera ya manunuzi ya umma kutoka Wizara ya Fedha Dk. Frederick Mwakibinga (kushoto) akisalimiana na Prof. Gaspar Munishi kutoka  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala wakati wa kongamano la kujadili rasimu ya Sera ya manunuzi ya Umma lililofanyika jana katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa JB jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo la siku moja lilihudhuliwa na wajumbe mbalimbali kutoka ofisi za Serikali na Taasisi binafsi.
Prof. Gaspar Munishi kutoka  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala akielezea  kuhusu rasimu ya Sera ya manunuzi  wakati wa kongamano hilo.
Baadhi ya wajumbe kutoka ofisi za Serikali na Taasisi binafsi wakimsikiliza Prof. Gaspar Munishi kutoka  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala (hayupo pichani) wakati wa kongamano la kujadili rasimu ya Sera ya manunuzi ya Umma lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Khamisi Tikka kutoka Mamlaka ya Rufaa za zabuni   akichangia mada  wakati wa kongamano la kujadili rasimu ya Sera ya manunuzi ya Umma lililofanyika jana katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa JB jijini Dar es Salaam.Picha zote na Anna Nkinda-MAELEZO

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.