
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mratibu wa mpambano huo wa raundi 6 kg,60 bondia wa siku nyingi ambae kwa sasa ni kocha wa mchezo huo Muheza, Chalres Muhilu ' Spins' alisema mpambano huo wa wazi umeandaliwa kwa ajili ya kutoa burudani wilayani hapo na kuhamasisha mchezo wa masumbwi
Katika mchezo huo kutakuwa na mapambano mengi ya utangulizi yatakayoanza saa kumi jioni ambapo hakutakuwa na viingilio.
Wapenzi wa mchezo huo wametakiwa kujitokeza kushuhudia mabondia kutoka Dar wakipambana na Muheza pamoja na kutoa rai kujitokeza kwa wafadhili kudhamini mchezo huo unaopendwa na vijana wengi wilayani humo.
Naye Kocha wa mchezo huo Rajabu Mhamila 'Super D' aliyepewa jukumu la kwenda na vijana kutoka Dar kutoa hamasa ya mchezo huo, amesema ataongozana mabondia, Nassoro Mbwiga, atakayemenyana na Bakari Sendekwa katika uzito wa kilo 52 na Iddy Mkwela atakaepambana na Lucas Ndula mpambano wa raundi 6.
No comments:
Post a Comment