BAADA ya kushikwa shati na maafande wa JKT Mgambo, katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliochezwa jana kwenye Uwanja wa CCM Mkwakwani, jijini Tanga, timu ya Yanga ambayo inafukuzia kwa karibu taji la Ligi Kuu ya Vodacom itashuka dimbani siku ya jumapili kupambana na JKT Ruvu katika mechi pekee ya ligi hiyo wikiendi hii itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Katika mchezo huo Yanga itakuwa na kibarua cha kuhakikisha inapata pointi tatu muhimu ili kunza shangwe za ubingwa mapema.
Mbali ya mechi hiyo, nyingine zitakazochezwa mwezi huu ni kati ya African Lyon na JKT Ruvu itakayofanyika Aprili 24 kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati Aprili 25 ni kati ya Ruvu Shooting na Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Nayo Coastal Union itaikaribisha Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga katika mechi itakayochezwa Aprili 27. Uwanja wa Taifa utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Simba na Polisi Morogoro itakayofanyika Aprili 28.

No comments:
Post a Comment