Greetings,
Please I need your urgent help at the moment..Am currently in Manila Philippines for a short program but unfortunately for me i can't withdraw money from my bank account over here,My (ATM)credit card decline due to some network problem.I contact my bank but they said till i get back home before the issue can be resolve at the bank headquarters..I am so confused right now,I don't know what to do or where to go.Please i need you to loan me $1,850 to sort myself here till i get back on Sunday..I promise to refund your money as soon as i get back home.
Let me know if this will be possible so I can forward you details on how you can get the funds to me.
I await your response
God bless
Ms. Bhanji
Mmiliki wa mtandao huu amekuwa akipata emails nyingi zinazoomba msaada wa kuwasaidia watu anaowafahamu huku zikionyesha kuwa wamekwama mahala fulani tena nje ya nchi, ili waweze kutumiwa kiasi cha fedha wanazokuwa wameziainisha.
Na jana mtandao huu ulipata email inayoonyesha kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shy-Rose Bhanji kuwa amepatwa na matatizo katika akaunti yake huku akihitaji msaada wa kutumiwa fedha kiasi cha Dola 1850 ili kusovu tatizo lake na kuahidi kurejesha pindi atakaporejea nyumbani.
Lakini kutokana na matatizo na uzoefu wa watu wanaofanya kazi hizi za kutapeli kupitia mitandao, inawezekana kweli mtu akawa na tatizo lakini watu wakaogopa kutoa msada huo.
Mtandao huu umelazimika kuchapicha ujumbe huu uliotumwa na email ya Shy-rose, ili kuwawezesha wadau kung'amua kama mtu huyu ni kweli ana matatizo na kweli yupo safarini katika nchi hiyo iliyotajwa ama ni wale wale? kila atakayesoma habari hii amjulishe na mwenzake tafadhali. Huenda ukapatikana ukweli. Wenu Sufianimafoto

No comments:
Post a Comment