Fuso lenye namba za usajili T 509 AGD, likiwa limeanguka na kumwaga mzigo wote wa Nyanya uliokuwa umebebwa na fuso hilo. Haikuweza kufahamika kwa haraka chanzo cha ajali hiyo.
Mmoja wa wahusika akijaribu kuomba msaada kwa magari yaliyokuwa yakipita eneo hilo.
Mafunzo wa Kampuni ya Strabag, wakiendelea na kazi ya upanuzi wa barabara ya Arusha inayoendelea kupanuliwa ambapo kwa sasa magari yamekuwa yakitumia muda mrefu kumaliza eneo hilo kwa kupita katika barabara vumbi iliyowekwa kwa dharula.
Upanuzi wenyewe ni kama hivi
Gari ndogo inayoelezwa kuwa iligongwa na basi la Happy Nations eneo la Mto Wami, likiwa limeegeshwa nje ya Kituo cha Polisi cha Wami.
Mafundi wakiendelea na ujenzi wa mitaro katika barabara mpya ya mabasi ya Kaskazini, inayotokea Bagamoyo.
Jamaa wakilinda mzigo wao nyuma ua Canter, kutoka Soko la Kariakoo kuelekea Tegeta.
haikuweza kufahamika jamaa hawa walikuwa wakisafiri kwa staili hii kuwa walikuwa na matatizo ya kijamii au ndo tatizo la usafiri, hapa wakitokea bagamoyo kuelekea Chalinze katika barabara mpya....
Ni baadhi ya wachezaji wa Taswa Fc, waliposhuka kupata chakula cha mchana maeneo ya Korogwe wakati wakielekea Mkoani Arusha kushiriki Bonanza linaloandaliwa na Taswa Arusha kila mwaka.
Safari hiyo ilijumuisha timu zote mbili ya Taswa Fc na Taswa Queens....
Wachezaji wakishuka garini kuelekea kupata msosi....
Maeneo ya mbali na mijini hivi ndivyo vituo vya mafuta ambapo huuzwa kwa lita moja moja kama hivi...
Mafuta aina ya Petroli, yakiuzwa kwa staili hii jambo ambalo ni hatari....













No comments:
Post a Comment