Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba Mh Sammuel Sitta amelazimika kuahirisha kikao cha bunge hilo leo jioni baada ya kutokea kutoelewana baina ya wajumbe ambao walianza kuzomea kama ilivyo kawaida yao. Mtafaruku huo umezuka baada ya baadhi ya Wajumbe na Baadhi ya wabunge wa upinzani kupinga Jaji warioba asiwasilishe rasimu ya katiba leo badala take asubiri hadi Rais atakapokuwa amezindua rasmi bunge hilo jambo ambalo lilizua mtafaruku wa sintofahamu huku wengine wakitaka Warioba kuwasilisha Rasimu baada ya Mhe. Rais Kulihutubia bunge hilo kwanza. Mwenyekiti wa Bunge akaruhusu Jaji Warioba aendeleee na Uwasilishaji lakini wabunge wakaanza kujibizana na kupiga makofi na meza za bunge huku wakizomea na baadhi ya wajumbe wakitoka nje na wengine wakisimama.
WAZIRI NANAUKA ATOA MAAGIZO KWA MAAFISA MAENDELEO YA VIJANA NCHINI
-
-Ataka Maafisa hao kuwa na takwimu sahihi za vijana
-Kuunganisha vijana na programu na fursa za Ujuzi, Ajira na Uwezeshaji
Kiuchumi
Na: Ofisi ya Rais, Mae...
1 hour ago

No comments:
Post a Comment