Habari za Punde

*KHALID CHOKORAA KUPANDA ULINGONI MAY 24 KUZIPIGA NA ABDUL MANYENZA

Mwanamuziki na kiongozi wa bendi ya Mapacha watatu, Khalid Chokoraa, anatarajia kupanda ulingoni jumamosi ya tarehe 24 katika ukumbi wa Friends Corner Manzese jijini Dar es Salaam,  kuzipiga na bondia chipukizi mwenye uchu wa ushindi  muda wote awapo ulingoni Abdul Manyenza. 

Chokoraa alisema muda mrefu amekuwa akifanya mazoezi ya  kujenga mwili na yahusuyo mchezo wa ngumi kwa ajili ya kujiandaa na pambano hilo huku akikutana na mabondia mbalimbali kupima uwezo wao.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Chokoraa alisema kuwa hivi sasa amejiandaa kuwathibitishia mashabiki wake kuwa ana vipaji tofauti tofauti kikiwamo cha ngumi.

''Nataka kuwaonyesha mashabiki wangu kuwa nina kipaji kingine zaidi ya kuimba, kama wengi walivyozoea kuniona nikiwa jukwaani nikipagawisha kwa sauti, na sasa nitawapagawisha kwa masumbwi''. alisema Chokoraa

Chokoraa amekuwa akijifua katika Gym ya Bigright Boxing iliyopo Mwananyamala  jijini Dar, chini ya mwalimu wake bondia  mkongwe Omar Athuman ‘Van Dame’ kwa lengo la kumsambaratisha mpinzani wake ambaye amekuwa akijitapa kumfanya Chokoraa, kuuchukia mchezo wa ngumi.

Pambano hilo litakuwa ni moja kati ya michezo ya utangulizi katika pambano la ubingwa wa UBO-Afrika kati ya Karama Nyilawila na Said Mbelwa.

Mapambano mengine ni kati ya Suleiman Galile akimkabili Abdallah Pazi, ‘kiroba’  Alan Kamote na Adam Ngange, Ramadhan Kumbele na Hassan Kiwale 'Morobest' ,  Idd Athuman na Julius Kisarawe, Zumba Kukwe wataoneshana kazi na Kamanda wa Makamanda.

Pia kutakuwa na mapambano mengine  ya utangulizi kati ya mabondia wa Tanga watakaozipiga na mabondia wa Dare es salaam, kama vile Athuman Boxa wa Tanga atazipiga na Waite Juma wa Chalinze, Rajabu Mahoja wa Tanga atazipiga na Kaisi wa Dar.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.