Habari za Punde

*TATIZO LA UMEME KUPATIWA UFUMBUZI IFIKAPO JUNI MWAKANI

NA MAGRETH  KINABO. MAELEZO
TATIZO la kutokuwepo umeme katika jijini Dares Salaam hususan maeneo ya katikati ya mji na nje kidogo ya mji na mkoa wa  Arusha, ikiwemo mikoa ya  Mwanza na Shinyanga linatarajiwa kupatiwa ufumbuzi ifikapo Juni mwaka 2015.

Hayo yalisemwa leo na  Mhandisi Mkuu wa masuala ya Umeme kutoka Benki ya Maendeleao ya Afrika(ADB), Dkt.  Babu  RAM  wakati akizungumza na waandishi wa habari leo(jana) mara baada ya  Waziri wa Fedha wa Marekani , Jack  Lew  ambaye aliwasili nchini usiku wa kuamkia leo(jana) na alitembelea nchini, jijini Dares Salaam kwa ziara ya siku moja ili kujionea shughuli mbalimbali  ukiwemo mradi wa ‘Electricity  V ‘ unaoendelea kwenye  Kituo kidogo cha kusambazia umeme kilijulikanacho kwa jina la Sokoine.

“ Mradi huu ni mojawapo ya agenda  ya  Serikali ya Tanzania ya matokeo makubwa sasa(BRN). Unahusisha ujenzi na uboreshaji wa vituo vidogo vya umeme vilivyoko katika jiji la Dar es Salaam na  mkoa wa Arusha, pia unahusisha upanuzi wa miundombinu ya usambazaji wa umeme katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga. Unaratajia kukamilika katikati ya mwaka 2015,” alisema  RAM.

Alisema mradi huo  katika kituo hicho , ambacho kinahusisha jiji la  Dares Salaam na mkoa wa Arusha kinatarajia kunufaisha mara mbili ya idadi ya sasa ambao ni  wateja 3000 na wafanyabiashara  wakubwa 400. Pia  wateja usambazaji wa umeme katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga utanufaisha wateja wapya 9000. 

“Mradi wote huu utanufaisha wateja wanakadriwa kufikia 12,000 na utagharimu Dola za Marekani milioni 50,” alisisitiza.

Alisema mradi huo utahusisha usambazaji wa umeme katika kituo kidogo cha  umeme  cha Ilala na mkoa wa Arusha kwenye eneo la Njiro.

Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa masuala ya umeme (nishati) kutoka  Wizara ya Nishati na Madini,  Mhandisi Innocent  Luoga alisema  mradi huo ni maojwapo wa Dira ya Maendeleo ya nchi ili ifikapo mwaka 2025 Tanzania iwe ni nchi ya kipato cha kati. 

Aliongeza kwamba mradi huo, utaongeza upatikanaji wa umeme kwenye maeneo ya katikati ya jiji la Dares Salaam, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Hospitali ya Ocean Road na Ikulu kwa sasa mahitaji ni makubwa kutokana na kuongezeka kwa majengo na jiji hilo kupanuka.

“Lengo kubwa la mradi huu ni mkakati wa Serikali wa kuongeza upatikanaji wa umeme katika jiji la Dares Salaam, Arusha,Mwanza,Shinyanga na maeneo ya vijijini,” alisema Luoga.

Luoga alisema  katika mradi huo, itawekwa transforma  yenye uwezo mkubwa  wa kufikia 30MVA  badala ya 15MVA zilizokuwepo hapo awali.

Alisema mradi huo unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika, ambayo inapata fedha kutoka Marekani kupitia mpango wa Rais wa Marekani, Barrack Obama wa miradi ya umeme (Power Africa Initiative),

Aliitaja miradi mingine, kuwa ni City Center unaofadhiliwa na Finland, Gongolamboto, Kurasini, Mkuranga, Mbagala, Kurasini, Kigamboni, Masaki, Mbezi, Ilala na Ubungo , ambapo itahusu upanuzi wa vituo na kuongeza transforma  kubwa.  
     
Katika ziara ya Waziri wa Fedha wa Marekani, Lew pia  alitemblea Wizara ya Fedha ,ambapo alifanya mazungumzo na   Waziri wa Fedha, Saada  Salum Mkuya, maeneo ya Bandari . kituo cha mafuta cha Kurasini na kufanya mazungumzo na viongozi husika.

Waziri huyo amefanya ziara hiyo katika nchi za Afrika ,ambazo ni Misri, Tanzania na Afrika ya Kusini , ambapo anatarajia kuwasili nchini humo baada ya kuondoka nchi leo usiku.

Lengo la ziara hiyo ni kuhimarisha uhusiano na nchi za Afrika kupitia baada ya ziara ya Rais wa Marekani, Barrack Obama  aliyoifanya mwaka jana katika nchi za Afrika  na kuzindua mpango huo.
Waziri huyo atarejea nchini kwake baada ya ziara ya Afrika Kusini. 
Mradi huo katika awamu ya kwanza  umehusisha nchi zingine ambazo ni  Kenya, Ethiopia,Ghana,Liberia  na Nigeria, ikiwemo Tanzania na una lengo la kunufaisha wateja zaidi ya milioni 60.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.