Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa Bw. Bernard Membe akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya
wizara yake kwa mwaka 2015/2016 bungeni leo mjini Dodoma.
Mabalozi wa Tanzania kwenye nchi mbalimbali
duniani wakifuatilia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa kwa mwaka 2015/2016 iliyowasilishwa leo bungeni mjini Dodoma.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dkt. Harrison Mwakyembe akimsikiliza kwa makini mbunge wa Bunge la Afrika
Mashariki Mhe. Makongoro Nyerere (kushoto) nje ya ukumbi wa bunge leo mjini
Dodoma. Kulia ni mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. ShyRose Bhanji.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju (kulia) akisisitiza jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati) kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma jana.
No comments:
Post a Comment