Marais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Uhuru Kenyatta wa Kenya wakipeperusha Bendera za nchi zao kuzindua ujenzi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Mwatate huko Taveta nchini Kenya leo.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya akimkaribisha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete eneo la TAVETA nchini Kenya muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuwasili na kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifunua vitambaa kuashiria kuanza ujenzi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Mwatate huko Taveta nchini Kenya leo. Rais Kikwete leo ameanza ziara ya kikazi ya siku tatu nchini Kenya.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya akifunua vitambaa kuashiria kuanza ujenzi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Mwatate huko Taveta nchini Kenya leo.
No comments:
Post a Comment