Habari za Punde

*TANZANIA YAJIPANGA KUTEKELEZA MPANGO MPYA WA MAENDELEO ENDELEVU (SDGs)

 Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akizungumza leo jijini Dar es salaam katika mkutano wa wadau wa takwimu uliondaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wenye lengo la kujadili na kukubaliana jinsi ya kutekeleza mpango wa Maendeleo Endelevu (SDGs).
 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa akizungumza katika mkutano wa wadau wa takwimu uliondaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wenye lengo la kujadili na kukubaliana jinsi ya kutekeleza mpango wa Maendeleo Endelevu (SDGs).
 Mwakilishi makazi wa benki ya dunia nchini Tanzania Ms. Bella bird akizungumza leo jijini Dar es salaam katika mkutano wa wadau wa takwimu uliondaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wenye lengo la kujadili na kukubaliana jinsi ya kutekeleza mpango wa Maendeleo Endelevu (SDGs).
Baadhi ya wadau wa takwimu wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue katika mkutano wa wadau wa takwimu uliondaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wenye lengo la kujadili na kukubaliana jinsi ya kutekeleza mpango wa Maendeleo Endelevu (SDGs).
****************************************
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue amesema Tanzania ina nafasi kubwa ya kufanikisha malengo ya Mpango wa Maendeleo Endelevu (SDGS).
Akizungumza na wadau wa Takwimu kwenye mkutano ulifanyika leo jijini Dar es salaam, Sefue amesema kutokana na Tanzania kufanya vizuri katika utekelezaji wa Malengo ya Milenia (MDGS) unaokamilika mwaka huu, ni hali inaoyonyesha kwamba Mpango huu mpya wa Maendeleo Endelevu utatekelezeka kwa ufanisi mkubwa.
 “Leo hii tupo hapa kwa pamoja kukubaliana ni jinsi gani tutaweza kufanikisha mpango mpya wa Maendeleo Endelevu (SDGs) baada ya kumalizika kwa utekelezaji wa Malengo ya Milenia (MDGs) ambao nchi yetu kwa kiasi kikubwa tumefanya vizuri,”amesema Sefue.
Sefue ameongeza kuwa, utekelezaji wa mpango huo mpya unahitaji uwepo wa takwimu za uhakika ambapo Tanzania inaendelea kuiboresha na kuiwezesha Ofisi ya Taifa ya Takwimu ili iendelee kutoa takwimu rasmi zitakazowezesha kupima utekelezaji wa mpango huu.
Sefue alisema utekelezaji wa mpango huu wa Maendeleo Endelevu kwa awamu hii unahitaji kila nchi kutoa ripoti ya utekelezaji wake kwa mwaka na hivyo itasaidia kufuatilia mafanikio ama changamoto zake kwa ukaribu.
Aidha, Sefue alisema kufanikiwa kwa Malengo Endelevu kutasaidia kuboresha maisha ya watanzania kutokana na malengo 17 yaliyopo kwenye mpango huo mpya kujikita katika uimarishaji wa hali ya maisha ya wananchi kwa ujumla.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Prof. Adolf Mkenda amesema kupitia Wizara ya Fedha, Serikali itahakikisha inaweka kipaumbele cha bajeti katika kufanikisha utekelezaji wa mpango huo.

“Tanzania imejipanga vizuri na kama ambavyo tulifanikiwa kutekeleza Malengo ya Milenia, tutatekeleza pia malengo haya mapya na kuboresha maisha ya wananchi wetu,” alisema Prof. Mkenda.
Mwezi Septemba mwaka huu, viongozi wa nchi mbalimbali duniani akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, walikutana nchini Marekani kwa ajili ya kutathmini utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia – MDGs ambapo ilionekana kwamba kuna baadhi ya malengo yalikuwa yamefanikiwa na mengine hayakufanikiwa.
Kutokana na hali hiyo, viongozi hao walikubaliana na kuridhia mpango mbadala wa MDG unaoitwa Mpango wa Maendeleo Endelevu ambao pia ni wa miaka 15 kuanzia 2015 hadi 2030 ambao Tanzania imeanza kuufanyia kazi.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.