Habari za Punde

*CHAMA CHA KUOGELEA CHAIPONGEZA SEMINA YA DAR SWIM CLUB

Hapa sasa ni Kazi Tu: Kocha wa Dar Swim Club, Michael Livingstone akiwafanyika mazoezi ya kuchumpa (ku-dive) waogeleaji wa klabu hiyo. Waogeleaji hao walifanya tendo hilo kwa staili mbalimbali baada ya kupokea mafunzo kutoka kwa makocha wa klabu maarufu ya Hamilton Aquatics, Nebojsa Durkin na Katy Morris. 
Mafunzo ya kuogelea siyo lazima yafanyikie kwenye maji. Hapa mkufunzi wa kimataifa wa mchezo wa kuogelea kutoka klabu ya Hamilton Aquatics, Nebojsa Durkin aionyesha kwa vitengo waogeleaji wa Dar Swim Club jinsi ya kuchumpa kwenye maji (ku-dive) katika mafunzo yaliyomalizika hivi karibuni kwenye shule ya Kimataifa ya DIA, Masaki. 
Mkufunzi wa kimataifa wa mchezo wa kuogelea kutoka klabu ya Hamilton Aquatics ya Dubai, Nebojsa Durkin aionyesha kwa vitengo waogeleaji wa Dar Swim Club jinsi ya kugeuka kwa kasi kwa kutumia nguvu ya miguu katika mafunzo yaliyomalizika hivi karibuni kwenye shule ya Kimataifa ya DIA, Masaki.
*****************************************
Chama cha mchezo wa kuogelea nchini (TSA) kimeipongeza klabu ya Dar Swim Club (DSC) kwa kufanya semina ya kuendeleza mchezo huo kwa wachezaji na makocha iliyokuwa chini ya wakufunzi kutoka klabu ya Hamilton Aquatics ya Dubai. 
Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Mkuu wa TSA, Ramadhan Namkoveka mara baada ya kutembelea mafunzo hayo yaliyofanyika kwenye bwawa la kuogelea la shule ya kimataifa ya DIA iliyopo Masaki jijini. 
Mafunzo hayo yalikuwa chini ya wakufunzi wa kimataifa wa mchezo wa kuogelea wa klabu bingwa ya Mashariki ya Kati (Middle East) ijulikanayo kwa jina la Hamilton Aquatics ya Dubai, Nebojsa Durkin na Katy Morris. 
Mafunzo hayo yalidhaminiwa na kampuni za Alios Finance Tanzania, Europcar, DSC, DIA na kampuni ya utafiti na uchimbaji wa mafuta ya Maurel & Prom. 
Wakufunzi hao walifuraishwa na viwango vya waogeleaji wa klabu hiyo pamoja na kukabiliana na changamoto mbalimbali za mchezo huo ikiwa pamoja na kukosa bwawa la mita 50 linalotambuliwa kimataifa. 
Namkoveka alisema kuwa wamefuraishwa na mafunzo hayo ambayo yaliwahusisha waogeleaji chipukizi (yoso) na wakubwa pia na makocha wa timu hiyo. Alisema kuwa wamevutiwa na jinsi mafunzo hayo yalivyokuwa yanaendeshwa na anaamini Tanzania itapata waogeleaji nyota kama wadau wa mchezo huo wataiga mfano wa DSC.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.