Habari za Punde

*TIMU ZA LIGI KUU KUVUNA ZAIDI YA MILIONI 120 MSIMU UJAO KWA MWAKA

 Na Ripota wa Sufianimafoto Blog, Dar
 SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu nchini TFF, limesaini mkataba wa miaka mitano na Kampuni ya Azam Media, wenye thamani ya Tsh. Bilioni 23 kwa kununua haki ya kurusha matangazo ya mpira wa ligi Kuu Tanzania Bara kuanzia msimu ujao wa  2016/17.
Katika mkataba huo kila timu  itavuka milioni 42 kwenye kila robo ya msimu na kwenye robo ya mwisho ambapo kila timu itapata fedha kulingana na nafasi yake kwenye msimamo wa ligi.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi mtendaji wa Azam Media, Tido Mhando, amesema kuwa mkataba huo umeboreshwa na kila timu sasa inatakiwa ifanye vizuri ili mwisho wa msimu iweze kupata fedha nyingi zaidi.
Katika msimu huu kumefanyika  marekebisho mapungufu yote yaliyojitokeza katika mkataba uliopita na hata kwenye baadhi ya mechi mliona kulikuwa na changamoto mbalimbali na tupo kwenye hatua za .mwisho kuzirekebisha.
"Pia kumekuwa na changamoto nyingi sana zilizojitokeza kipindi cha mkataba wetu wa awali lakini tumezifanyia kazi na kwa sasa zipo kwenye hatua za mwisho za kuzimalizia ikiwemo vifaa na hata majukwaa ambayo yatakayokuwa yanatumika kwa ajili ya kuwekea camera kwani viwanja vingi sio rafiki kwa kazi yetu, "alisema Mhando.

Kwa upande wa TFF, Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi Boniface Wambura alisema kuwa hii ni hatua nzuri kwao pia na hata kwa vilabu kwani mkataba umeboreshwa ambapo katika Msimu ujao timu zote zitafaidika sana. Mkataba huu wa miaka mitano kwa mwaka kila timu itachukua zaidi ya milioni 120.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.