Nairobi, Kenya:
SAA chache baada ya kusambaa mitandaoni kwa video inayomuonesha gwiji wa muziki wa dansi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Koffi Olomide akimpiga mateke mmoja kati ya madansa wake wa kike, msanii huyo ameibuka na kukanusha madai hayo na kueleza kwamba alikuwa akiwalinda madansa wake wasiibiwe lakini hiyo haijazuia serikali ya nchi hiyo kumtimua.
Katika tukio hilo lililotokea muda mfupi baada ya Koffi kutua uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi akiwa na madansa wake, nguli huyo anaonekana akimvurumishia mateke dansa huyo huku maafisa wa polisi waliokuwa uwanjani hapo wakimtuliza.
“Mimi ni mtu ninayewaheshimu wanawake, siwezi kufanya tukio kama hilo. Kilichotokea ni kwamba nilikuwa nikifanya mahojiano na waandishi wa habari, nikasikia kelele nyuma yangu. Kugeuka nikamuona mtu mmoja ambaye baadaye niliambiwa ni kibaka wa mifukoni, akitaka kuwaibia madansa wangu, ikabidi nimrushie teke ili kumzuia asiwaibie,” alisema Koffi katika mahojiano maalum na Kituo cha Runinga cha Citizen.
No comments:
Post a Comment