Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura akionyeshwa eneo litakalo jengwa kituo cha mafunzo ya michezo leo jijini Arusha leo na Katibu Mkuu wa Trust St.Patrick Sport Academy Bi.Dinna Patrick alipotembelea eneo hilo kujionea hali halisi.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura(katikati) akitoa maagizo leo jijini Arusha kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa Bi Alice Mapunda(wakwanza kushoto) kuhusu barabara iliyopita katikati ya mradi huo wa kituo cha mafunzo ya michezo.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Annastazia Wambura akisalimiana na Mwanariadha wa zamani Bw.Faustine Sulle ,mara baada ya mkutano wa wadau wa kisekta uliyofanyika jijini Arusha katika ofisi za Mkuu wa Mkoa.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Annastazia Wambura (watano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja leo jijini Arusha na baadhi ya wanafunzi wa wasichana katika Shule ya Trust St.Patrick Sport Academy wanaocheza mpira wa alipotembelea shule hiyo inayofundisha michezo mbalimbali ,wanne kulia ni Meneja wa Shule hiyo Bw.Patrick Khagya.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Annastazia Wambura (watano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja leo jijini Arusha na baadhi ya wanafunzi wa wanaocheza mpira wa kikapu katika Shule ya Trust St.Patrick Sport Acadealipotembelea leo jijini Arusha kujionea timu zao za michezo,watatu kushoto ni Katibu Mkuu wa Shule Bi.Dinna Patrick. Na
Anitha Jonas – MAELEZO,ARUSHA
**************************************************
Anitha
Jonas – MAELEZO
Serikali
ya pongeza uongozi wa Trust St.Patrick Sport Academy kwa uamuzi wa kujenga Kituo cha Mafunzo ya Michezo chenye
hadhi ya Kimataifa.
Pongezi
hizo zimetolewa leo jijini Arusha na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni ,Sanaa na
Michezo Mhe. Anastazia Wambura alipotembelea eneo hilo litakalojengwa kituo
hicho ambacho kitakuwa na Michezo ya aina mbalimbali pamoja na hoteli ya nyota
tano.
“Serikali
inaunga mkono jitihadi za ujenzi huu kwani kituo hichi kitakapo malizika
tunaimani kitakuwa chachu ya ukuaji wa
vipaji vya michezo kwa watanzania na kutaongeza mafanikio ya sekta ya michezo
na kuwezesha kupata ushindi katika michezo mbalimbali katika ngazi za
Kimataifa,”alisema Naibu Waziri.
Naye
Katibu Mkuu wa Kituo hicho Bi.Dinna Patrick
alimweleza Naibu waziri huyo chagamoto waliyonayo katika eneo hilo la kuwepo kwa barabara
inayogawa eneo hilo la kituo hicho ambalo ndiyo limekuwa kikwazo kinacho
kwamisha ujenzi wa kituo hicho kuanza kwa haraka.
“Kituo
hicho kitakuwa na uwanja wa mpira ambao utakuwa na uwezo wa kuchukua watu elfu
ishirini ambao utakuwa wenye hadhi ya kimataifa na kituo hicho kinatarajiwa
kuwa bora zaidi katika Kanda ya Afrika
Mashariki”,alisema Bi.Patrick.
Baada
ya kupata malalamiko hayo Mheshimiwa huyo aliuagiza uongozi wa mkoa kufuatilia suala hilo katika ofisi za
Halimashauri na kusaidia suala hilo kupata ufumbuzi ili kuharakisha ujenzi wa
eneo hilo kwani kumalizika kwake kutaleta faida kubwa kwa wapenzi wa michezo.
Aidha
,Naibu waziri huyo alitoa wito kwa uongozi wa Trust St.Patrick Sports Academy
kujenga pia chuo cha walimu wa michezo mbalimbali nchini kwani kuna changamoto
kubwa ya ukosefu wa walimu wa michezo na uhaba wa vyuo vya michezo nchini.
Hata
hivyo watanzania wenye uwezo wametakiwa kujitokeza na kujenga vituo vya mafunzo
ya michezo kwani michezo ni ajira na inaweza kuchangia pato kubwa katika nchi.
No comments:
Post a Comment