Habari za Punde

*SERIKALI YAIPONGEZA BENKI YA STANDARD CHARTERD

Na: Frank Shija, MAELEZO
Serikali imeipongeza Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa kupeleka huduma za kibenki kwa wananchi wanao ishi katika maeneo ambayo benki hiyo haina matawi hapa nchini.
Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa.Makame Mbarawa katika hafla fupi ya Iftari iliyoandaliwa na Benki hiyo jana Jijini Dar es Salaam.
Mbarawa amesema kuwa Sekta ya Benki ni muhimu kwa jamii hivyo kwa Standard Chartered Tanzania kupeleka huduma zao kupitia ushirikiano baina yao na Benki ya Posta katika matawi yake pote nchini.
“Nawapongeza sana kwa kuona haja ya kushirikiana na Benki ya Posta ili kuwapelekea huduma wananchi wengi zaidi katika maeneo ambapo hamna matawi yenu.”Mbarawa.
Aidha Mbarawa alitumia fursa hiyo kuwata Waumini wa dini ya Kiislamu na wananchi kwa ujumla kuwa na mahusiano mema ili kudumisha amani.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered Tanzania Sanjay Rughani amesema kuwa Benki yao imeona umuhimu wa kupanua wigo wa huduma zao kutokana na kuwa na matawi machache nchini nzima.
Aliongeza kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya kusikia uhitaji wa wananchi hususan wakazi wa Arusha ambao waliomba kuongezewa matawi ya Benki hiyo kutoka tawi moja lililopo sasa.

Benki ya Standard Chartered Tanzania imeingia ubia na Benki ya Posta Tanzania ili kutoa huduma za kibenki kupitia matawi ya Benki ya Posta popote yalipo nchini na kwa kufanya hivyo kunatoa fursa kwa wananchi wengi zaidi kunufaika na huduma za Benki ya Standard Chartered Tanzania.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.