Habari za Punde

*SIMBA APIGWA 2-0 NA JKT RUVU KATIKA FAINALI ZA FASDO CUP JIJINI DAR

Kikosi cha timu ya Simba chini ya Umri wa Miaka 20 katika picha ya pamoja kabla ya mchezo dhidi ya JKT Ruvu, kuanza.
Kikosi cha timu ya JKT Ruvu chini ya umri wa miaka 20 katika picha ya pamoja.
Mkurugenzi mtendaji wa Faru Arts and Sport Development Organization (FASDO) Tedvan Chande Nabora akikagua timu zote mbili kabla ya mchezo huo. 
Mtanange ukiendelea.
Mtanange ukiendelea
Mchezo huo ukiendelea; Katika mchezo huo JKT Ruvu waliibuka washindi kwa mabao 2-0 dhidi ya Simba, huku Simba wakikosa penalti.
Mgeni Rasmi katika Mashindano hayo ya FASDO, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mh. Humphrey Polepole akifuatilia Mchezo huo 
Mashabiki wa upande wa Simba wakifuatilia kwa makini Mchezo huo
Mashabiki upande wa JKT Ruvu wakiwa wanafuatilia kwa makini mchuano huo 
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, akifurahia kikombe
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mh. Humphrey Polepole akionesha kombe pamoja na zawadi ya mshindi wa kwanza kiasi cha Tsh 2,000,000 wakati wa fainali hizo, zilizofanyika katika viwanja vya JK jijini Dar es Salaam.
Mwamuzi Bora katika mashindano hayo ya FASDO akikabidhiwa zawadi ya Kitita cha 100,000.
Nahodha wa Timu ya Simba U20, akipokea zawadi yao ya mshindi wa pili katika Michuano hiyo,   Tsh 1,000,000.
Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mh. Humphrey Polepole akikabidhi zawadi ya mshindi wa kwanza kitita cha Tsh 2,000,000 kwa Nahodha wa timu ya JKT Ruvu ambao ndio waliibuka kidedea.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mh. Humphrey Polepole akikabidhi Kombe kwa mshindi timu ya JKT Ruvu baada ya kuibuka washindi
Wakiwa wanalipokea rasmi kombe lao baada ya ushindi 
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mh. Humphrey Polepole (Kulia) akikabidhiwa zawadi ya picha kutoka taasisi isiyo ya kiserikali ya FASDO
Timu ya JKT Ruvu wakifurahi baada ya kuibuka washindi.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.