Habari za Punde

BRAC yahimiza uwekezaji katika uwezeshaji wa wasichana na wanawake katika Mkutano wa Kimataifa wa Women Deliver 2023




Na Mwandishi Wetu

Shirika la maendeleo la kimataifa ambalo linafanya kazi zake Afrika na Asia, limeendelea kusisitiza ahadi yake ya kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji kwa wasichana na wanawake ili kubadilisha maisha yao na jamii.


Hayo yamesemwa katika Mkutano wa Women Deliver 2023 uliofanyika Kigali, Rwanda kutoka 17 hadi 20 Julai. Mkutano wa Women Deliver ni jukwaa la kimataifa ambalo linakutanisha na wanaharakati, watunga sera, watetezi, na wadau kujadili usawa wa kijinsia na afya, haki, na ustawi wa wanawake na wasichana. 


Mkutano huo ulizungumzia maswala makubwa na ulilenga kutambua suluhisho za vitendo ili kuendeleza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake. BRAC ilionyesha njia zinazotekelezwa katika kusaidia wasichana na wanawake vijana kubadilisha maisha yao na jamii. Kwa kauli mbiu ya 'Power Her Potential', shirika hilo lililenga kuongeza uelewa juu ya haja ya haraka ya hatua za pamoja kuwekeza katika uwezeshaji wa wasichana na wanawake.


Moja wa washiriki wa Mkutano huo , Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ya Tanzania Dorothy Gwajima 

alisema, "Nchini Tanzania, tunajitahidi kuhakikisha sauti ya wasichana na wanawake vijana inainuliwa vya kutosha, na wanaathiri maamuzi ya sera"


Naye, Mkurugenzi wa Kimataifa wa Jinsia, Benki ya Dunia,  Hana Brixi alisema "BRAC ni mshirika mkubwa wa Benki ya Dunia na chanzo kikubwa cha msukumo chanya; wanaonyesha kile kinachofanya kazi na tunaweza kusaidia kufanya kazi hiyo kwa mamilioni ya wanawake pamoja."

Kikao hicho kilifungwa kwa maneno kutoka kwa, Mkurugenzi wa Kanda - Afrika,  BRAC International, Rudo Kayombo alizungumzia juu ya hatua zinazofaa za umri kwa wasichana wadogo na kuahidi Kuwafikia kwa zaidi. Amesema lazima waanze  kuwafikia watu mapema kwa sababu vinginevyo hatutafikia malengo."


Ushiriki wa BRAC katika mkutano huo pia ulijumuisha nafasi ya maonyesho, kikao cha wakati huo huo, na mazungumzo katika siku za mkutano, kuonyesha na kutetea njia ya maendeleo ya ili kuunda athari chanya kwa watu wengi.

BRAC imekuwa ikifanya kazi nchini Tanzania tangu mwaka 2006 ikiwafikia zaidi ya watu milioni 5. Nchini Tanzania, BRAC ina taasisi ya maendeleo ya jamii na taasisi ya fedha. BRAC Maendeleo Tanzania inafanya kazi kwa ajili ya mipango ya maendeleo ya jamii kwa kuchukua njia shirikishi, ya jamii, na ya umoja wa kubuni mipango maalum ya mazingira, yenye athari chanya. 


BRAC Tanzania Finance Ltd ni taasisi kubwa zaidi ya fedha nchini Tanzania inayotoa huduma mbalimbali za kifedha kwa watu walio chini ya piramidi, kwa kuzingatia hasa wanawake wanaoishi katika hali ya umaskini katika maeneo ya vijijini na maeneo magumu kufikia.


 Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Jeannette Bayisenge, Waziri wa Jinsia na Ukuzaji wa Familia nchini Rwanda; Ingabire Assumpta, Waziri wa Nchi wa Serikali ya Rwanda; Williametta Saydee-Tarr, Waziri wa Jinsia, Watoto na Ulinzi wa Jamii wa Liberiaa;  Natalia Kanem, Mkurugenzi Mtendaji, UNFPA;  Anita Zaidi, Rais, Idara ya Usawa wa Jinsia, Bill & Melinda Gates Foundation; Hana Brixi, Mkurugenzi wa Kimataifa wa Jinsia, Benki ya Dunia; Rudo Kayombo, Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika, BRAC International.


BRAC ilianzishwa nchini Bangladesh mwaka 1972. Shirika hilo linafanya kazi katika nchi 17 barani Afrika na Asia, likishirikiana na watu zaidi ya milioni 100 duniani kote wanaoishi na ukosefu wa usawa na hali ya umaskini ili kutengeneza fursa za kutambua uwezo na kufikia uwezo wao.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.