WAKATI Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Mstaafu, Said Kalembo, akitangaza kula sahani moja na Wazungu wanaorandaranda mitaani hovyo bila shughuli maalum na kuwakamata katika Mkoa huo, hapa jijini Wazungu kibao wametapakaa katika mitaa ya uswahilini kiasi cha kupishana nao kama majirani tena katika mitaa ambayo huzanii kukutana nao.
Kamera ya Sufianimafoto leo ilifanikiwa kuwanasa wazungu hao wakiingia katika Mgahawa wa Uswazi huko mitaa ya Mkwajuni Hananasifu, huku wakiwa wamepiga pensi zao na mmoja akiwa ametinga malapa chini, huku wakipiga stori na kuzama katika mgahawa huo uliopo Barabara ya Katumba karibu kabisa na barabara kubwa ya Kawawa.
Kamera ya Sufianimafoto leo ilifanikiwa kuwanasa wazungu hao wakiingia katika Mgahawa wa Uswazi huko mitaa ya Mkwajuni Hananasifu, huku wakiwa wamepiga pensi zao na mmoja akiwa ametinga malapa chini, huku wakipiga stori na kuzama katika mgahawa huo uliopo Barabara ya Katumba karibu kabisa na barabara kubwa ya Kawawa.
No comments:
Post a Comment