Habari za Punde

*SHIRIKA LA NDEGE LA QATAR KUPANUA WIGO NA KUBORESHA HUDUMA ZAKE AFRIKA MASHARIKI

Safari za mara kwa mara za nchini Kenya na Tanzania na nyongeza ya safari 12 kwa wiki, kwenda Nairobi mara mbili Kwa siku, safari tano zaidi kwa Dar es Salaam.

Shirika la ndege la Qatar leo limetangaza kupanua mtandao wake wa Afrika Mashariki kwa kuongeza safari 12 zaidi kupitia miji mikuu miwili – Dar es Salaam na Nairobi.

Mji mkuu wa Tanzania, Dar es Salaam, hivi sasa una huduma kila siku, kupata nyongeza ya safari nne kwa wiki kutoka mwezi Januari. Safari za nyongeza kuanzia Februari 14 zitachukua mzunguko hadi wiki 12 za huduma.

Safari za kila siku kutoka Nairobi kwenda Doha zimeongezeka hadi kufikia safari 12 kwa wiki. Kuanzia tarehe 3 mwezi Januari safari za nyongeza mbili zitachukua nafasi hadi mara mbili kwa siku.

Safari zote zinatolewa na ndege aina ya A320 zikiwa na viti 12 vya daraja la pili na viti 132 daraja la tatu.

Bara la Afrika ni mojawapo ya soko kubwa la Shirika la ndege la Qatar kwa idadi ya vituo linavyohudumia na mji pekee kutengeneza zaidi ya asilimia10 ya mtandao wa kimataifa wa shirika hilo.

Shirika la ndege la Qatar hivi sasa linasafiri katika miji 14 Afrika, ikiwemo Alexandria, Aljeria, Misri, Luxor, Casablanca, Cape Town, Johannesburg, Khartoum, Lagos, Nairobi, Dar Es Salaam, Shelisheli, Tripoli na Tunisia.

Kutoka kila mji, Shirika linatoa ofa kwa kupitia kiungo chake cha Doha kufikia vituo vingi kwenye mtandao wake Ulaya, Mashariki ya kati, Asia kusini na kaskazini pamoja na Amerika ya kusini.

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la ndege la Qatar Bw. Akbar Al Baker alisema "Tunayo furaha kutambulisha upatikanaji wa safari za nyongeza kwa Afrika na kutoa ofa kubwa ya kwa abiria kuchagua ndege kutoka na kwenda kwenye miji.

“Kama sehemu ya mkakati wa ukuaji wetu, tunaendelea kupiga hatua mbele katika safari za mara kwa mara, katika vituo ambapo ni hatua madhubuti kuongeza ukuaji wetu katika nyanja za biashara na Utalii.

“Safari ya Dar es Salaam limefanya vizuri zaidi kwa kipindi cha miaka mine iliyopita ambapo ilizinduliwa mwezi Januari mwaka 2007”

“Mara kwa mara tumekuwa tukihudumia Nairobi tangu mwezi Novemba mwaka 2005 na hii imekua moja ya historia ya mafanikio makubwa Afrika, kwa hiyo tunayofuraha kuwapatia abiria wetu nafasi zaidi kwa kuongeza safari hadi kufikia mara mbili kwa siku,” aliongeza.

Zaidi ya miezi minne ijayo, ukuaji wa shirika utalenga Ulaya likiwa na vituo vipya vinne vitakavyotambulishwa– Budapest (Januari 17), Bucharest (Januari 17), Brussels (Januari 31), na Stuttgart (Machi 6), kabla ya kuzindua kituo chake cha 100 kwa mji wa Syria wa Aleppo tarehe 6 Aprili.

Hivi karibuni shirika linaendesha safari zake za ndege 93 katika vituo vikubwa vya biashara kupitia Ulaya, Mashariki ya kati, Afrika, Asia Pacific, Amerika ya kaskazini na Kusini. Kituo kipya kilichoongezwa ni Meditterrania ya Ufaransa tarehe 24 mwezi Novemba.

Kufikia mwaka 2013 Shirika la ndege Qatar linapanga kutoa huduma katika vituo 120 ulimwenguni likiwa na lengo la wastani wa ndege 120 kwa kipindi cha miaka mitatu.

Ratiba ya safari mpya za Afrika Mashariki

DAR ES SALAAM - DOHA
Jumatutu, Jumatano, Alhamisi na Jumapili – kuanzia Januari 2
Kuondoka Dar Es Salaam QR547 saa 1815, kufika Doha saa2350
kuondoka Doha QR546 at 1120 saa, kufika Dar Es Salaam saa 1715

Jumamosi – kuanzia Februari 14
Kuondoka Dar Es Salaam QR547 saa 1815, kufika Doha saa 2350
Kuondoka Doha QR546 saa 1120, kufika Dar Es Salaam saa1715

NAIROBI - DOHA
Jumatatu, jumatano, Alhamis, Jumamosi na Jumapili
Kuondoka Nairobi QR535 saa 1850, kufika Doha saa 2345
KUondoka Doha QR534 saa 1230, kufika Nairobi saa 1750

Jumanne na Ijumaa – kuanzia Januari 2
Kuondoka Nairobi QR535 saa 1850, kufika Doha saa 2345
Kuondoka Doha QR534 saa 1230, kufika Nairobi saa 1750

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.