Mfanyabiashara wa visu vya kukunia Nazi, vinavyofanya shughuli zaidi ya moja, akionyesha jinsi visu hivyo vinavyofanya kazi ili kuwavutia wateja wake kama alivyokutwa na Sufianimafoto pembeni mwa Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam, visu hivyo huuzwa kwa Sh. 1500 hadi 2000.
Wakazi wa jijini Dar es Salaam, wakichagua viatu kwa mchuuzi wa biashara hiyo jijini Dar es Salaam. Pamoja na agizo la Manispaa za jijini kuwataka wafanyabiashara hao kutopanga biashara zao pembezoni mwa barabara, agizo hilo linaonekana kupuuzwa kwani wafanyabiashara hao wamezidi kumiminika katika maeneo mbalimbali ya jijini na kuendelea na biashara zao.
Huu ndiyo msimu wa matunda kama unavyoona pichani ni Nanasi zikiwa zimejaa kwenye Soko la Buguruni Dar es Salam. Kwa sasa kila nanasi moja huuzwa kwa sh. 300, 500 hadi 1000.
Hii ni noma washkaji kukojoa mahali kama hapa hadhalani namna hii.......
No comments:
Post a Comment