Ofisa Operesheni wa Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma PPF, Kanda ya Temeke, Linda Njoolay, akigawa sehemu ya msaada kwa Asha Arabi mkazi wa Mbagala Rangi 3 aliyelazwa kwenye Wodi ya watoto katika Hospitali ya Wialaya Temeke Jijini Dar es Salaam jana, wakati Meneja wa Lindi na Mtwara, Lulu Mengele na ujumbe wake walipofika hospitalini hapo kukabidhi vifaa vya kuhifadhia maji (Sim Tank) mbili zenye thamani ya Sh. milioni 2 kila moja likiwa na uajazo wa Lita 500 kwa ajili ya kusaidia tatizo la maji katika wodi ya wazazi na Chumba cha upasuaji.
Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma PPF, Kanda ya Temeke, Lindi na Mtwara, Lulu Mengele, akifurahi na mtoto Janeth Gaudence, baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali katika wodi ya watoto hospitalini hapo leo mchana. Kushoto ni mama wa mtoto huyo, Editulda Gaudence.
Wauguzi na wafanyakazi wa PPF wakiwa bize kugawa sehemu ya misaada hiyo ndani ya wodi ya watoto.

Hawa ni baadhi ya wadau na waandishi wa habari waliohudhulia hafla hiyo kwenye Hospitali ya Wilaya ya Temeke leo.
No comments:
Post a Comment