Habari za Punde

*NI LINI WABONGO TUTAKUA NA UELEWA NA KUZINGATIA USAFI WA MAZINGIRA KAMA NCHI ZA WENZETU?

Pamoja na jitihada kibao za Manispaa za jiji kuweka vifaa vya kuhifadhia taka katika baadhi ya maeneo ya jiji hili, lakini bado Wananchi hawana utaratibu wa kujizoesha kutumia vifaa hivyo kama picha hii inavyoonesha, pamoja na kuwapo kifaa cha kuhifadhia taka lakini bado watu wasiojulikana wamefika mahala hapa na kutupa taka zao mtaroni na pembeni mwa kifaa hicho. Je namna hii tutafika kweli na jitihada za kuweka jiji safi?

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.