Habari za Punde

*VODACOM TANZANIA YADHAMINI MASHINDANO YA UVUVI KISIWA CHA SINDA

 Wafanyakazi wa boti ya Mistress wakiwa wamebeba samaki walizovua katika kisiwa cha Sinda wakati wa mashindano ya uvuvi  yajulikanayo kama Latham Open yaliyoshirikisha nchi sita  na kudhaminiwa na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania, yaliyomalizika mwishoni mwa wiki.
Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania, George Rwehumbiza (kulia) akitoa zawadi kwa mshindi wa uvuvi kwa upande wa watoto Kyle Balarin (15) aliyekuwa akitumia boti  ya Tarka katika mashindano yaliyofanyika kisiwa cha Sinda mwishoni mwa wiki, (katikati) ni Commodore Spiras Manoloudis wa Yatch Club akishuhudia utoaji wa zawadi hizo.
Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania Bw. George Rwehumbiza (kulia) akimkabidhi zawadi  Alfred Charles kwa niaba ya timu yake baada ya kuibuka washindi wa kwanza kwa upande wa boti ya Mistress katika mashindano yaliyofanyika huko Sinda kisiwani mwishoni mwa wiki na kudhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania.
Kikundi cha Sanaa cha Jambo brothers kutoka Zanzibar kikionyesha sarakasi mbalimbali katika kisiwa cha Sinda wakati wa mashindano ya uvuvi (latham Open) yaliyokuwa yakiendelea kisiwani humo, ambayo pia  yalidhaminiwa na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.