Habari za Punde

*STARS MPYA YA KIM POULSEN YAANZA NA SARE YA 0-0 MECHI YA KIRAFIKI NYUMBANI

 Kikosi kipya cha timu ya Taifa Stars, kilicho chini ya Kocha mpya Kim Poulsen, kilichocheza mechi ya Kirafiki ya Kimataifa na Malawi leo katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam na kutoka sare ya bila kufungana.
 Kiungo wa Taifa Stars, Mwinyi Kazimoto (kulia) akimiliki mpira mbele ya mchezaji wa timu ya Taifa Malawi, James Sangala, wakati wa mchezo wa Kirafiki wa kimataifa baina ya timu hizo, uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam leo jioni. Timu hizo zimetoka sare ya 0-0.
 Kiungo Mshambuliaji wa Taifa Stars, Haruna Moshi 'Boban' (kulia) akijiandaa kumtoka beki wa Malawi, Limbikani Nzava, wakati wa mchezo huo.
 Mshambuliaji wa Taifa Stars, Mrisho Ngasa (katikati) akiwatoka mabeki wa Malawi, wakati wa mchezo huo.
Mshambuliaji wa Kimataifa wa timu ya Taifa Stars, Mbwana Samatta (kulia) akimhadaa beki wa Malawi, wakati wa mchezo huo.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.